MWANARIADHA wa kike ambaye alimaliza mashindano ya
marathon yaliyofanyika jijini London mwishoni mwa wiki iliyopita anahofiwa
kutoroka ili kukwepa kurudi nyumbani kwao Sierra Leone. Mwanadada huyo
Mami Konneh Lahun mwenye umri wa miaka 24 mara ya mwisho alionekana baada ya
kumaliza mbio za kilometa 42 jana na alitakiwa kurejea nchini kwake
leo. Polisi walilazimika kuanza kumsaka baada ya Lahun kushindwa kurejea
katika makazi yake ya muda huko Greenwich jana. Mwanadada huyo ndio
mwanariadha mwenye kasi zaidi katika mbio za mita 5,000 na 10,000 nchini Sierra
Leaone na mwanamke wa kwanza kuiwakilisha nchi hiyo katika mbio za London
marathon. Tabia za wanariadha kujificha baada ya mashindano na baadae
kuomba hifadhi ya kisiasa na kuishi kama wakimbizi limekuwa ni jambo la kawaida
katika mashindano makubwa. Katika michuano ya olimpiki iliyofanyika jijini
London mwaka 2012 wanariadha wengi na makocha walitoroka au wengine kuomba
hifadhi za kisiasa kutoka hali machafuko nchini katika nchi wanazotoka.
No comments:
Post a Comment