NGULI wa soka wa zamani wa Cameroon, Roger Milla
amepoteza rekodi yake ya kuwa mchezaji mzee zaidi kuiwakilisha nchi yake barani
Afrika kwa mshambuliaji wa Mauritius Kersely Appou mwenye umri wa miaka
43. Milla alijiwekea rekodi hiyo wakati alipofunga bao katika mchezo
Cameroon waliofungwa na Urusi mabao 6-1 katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka
1994 akiwa na umri wa miaka 42 na siku 39. Bado anashikilia rekodi yake ya
kuwa mchezaji mzee na kufunga bao katika michuano ya Kombe la Dunia. Appou
alicheza katika kikosi cha Mauritius kilichofungwa na Mauritania katika mechi
ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika Jumamosi iliyopita. Mshambuliaji
ana umri wa miaka 43 na siku 354, umri ambao bado haujafikia wa mchezaji wa
Visiwa vya Virgin McDonald Taylor anayeshikilia rekodi ya kwa kuwa mchezaji
mzee zaidi kwa kucheza akiwa na umri wa miaka 46 na siku 217.
No comments:
Post a Comment