ACHOMWA KISU NA MWANAMKE ALIYETAKA
KUMBAKA
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Evarist Mangalla |
Mtu
mmoja aliyejulikana kwa jina Stephen
Philbert(30) mkazi wa Ngokolo mjini Shinyanga ameuawa kwa kuchomwa kisu wakati
akifanya jaribio la kumbaka mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 24 katika eneo
la Ngokolo mjini Shinyanga usiku wa mkesha wa pasaka.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Evarist Mangalla amesema kuwa tukio hilo
limetokea Aprili 20 ,mwaka huu saa tisa usiku.
Amesema
siku ya tukio mwanamme huyo alivunja dirisha la nyumba ya mwanamke huyo
na kuingia ndani kisha kufanya jaribio la kumbaka lakini katika kujihami kwake
ndipo mwanamke huyo alimchoma kisu kichwani ,akafariki dunia akiwa katika
hospitali ya mkoa wa Shinyanga.
Jeshi
la polisi linamshikilia mwanamke huyo kwa mahojiano zaidi.
No comments:
Post a Comment