HUU NI UNYAMA, AFISA WA POLISI ADAIWA KUMUINGIZA CHUPA YA BIA SEHEMU ZA SIRI MKEWE
MJAMZITO
MWANAMKE
MMOJA mjamzito anauguza majeraha katika Hospitali ya Meru Level Five nchini
Kenya baada ya kudaiwa mumewe aliingiza chupa kwenye sehemu zake za siri.
Mama
huyo mwenye umri wa miaka 31 alisemekana kupigwa na mumewe, ambaye anahudumu
kama Konstebo katika kambi ya polisi wa utawala ya Gatimbi, Kaunti ndogo
ya Imenti.
Akieleza
masaibu yake akiwa hospitalini, mama huyo alisema mumewe aliyekuwa mlevi
aliwasili nyumbani mwendo wa saa tisa alfajiri Jumamosi na kumwagiza avue nguo
zote akiwa nje.
Alisema
alitii maagizo hayo na polisi huyo akavaa sare yake ya kazi, akachukua chuma na
risasi mbili kisha kumpiga na kusema kwa sauti kuwa ataua mtu siku hiyo.
“Hapo ndipo alipochukua chupa ya pombe
aliyokuwa amebeba na chuma, akaziingiza kwenye sehemu zangu za siri.
Alinifunika mdomo ili nisipige kelele,” alieleza huku akidondokwa na machozi.
Alizimia
kwa saa kadha ndani ya nyumba huku akivuja damu nyingi.
“Niliamka
mwendo wa saa 11.30 na kumpata akiwa amelala kitandani, pengine alizidiwa na
pombe nyingi aliyokunywa. Nilitambaa hadi makao makuu ya kambi ambapo maafisa
wengine walinikimbiza hadi hospitalini,” alisema.
Baadaye
alilazwa katika zahanati ya Gatimbi ingawa alihamishwa hadi hospitali ya Meru
baadaye ili kupokea matibabu maalum.
Kulingana
na Dkt Jamal Mohamed ambaye ni daktari katika hospitali hiyo, hayuko taabani
kwa sasa ingawa bado anahitaji kutazamwa kwa makini.
“Tunamtibu pia kutokana na matatizo ya kiakili
aliyopata ingawa anaendelea vyema,” alisema.
Akithibitisha
mkasa huo, Kamanda wa polisi wa utawala katika Kaunti ya Meru, Bw Njue Njagi,
ambaye alimtembelea hospitalini alisema huenda wawili hao walikuwa na ugomvi wa
kinyumbani kabla tukio hilo kutendeka.
Alisema
mshukiwa huyo ambaye hakuwa amekamatwa wakati huo, atashtakiwa baada ya polisi
kukamilisha uchunguzi wao.
Bw
Njagi alisema afisa huyo ameagizwa kufika afisini na kuongeza kuwa agizo la
kukamatwa kwake litatolewa ikibainika alikuwa na hatia.
“Hatujatambua
kilichotokea kabla tukio hilo lakini uchunguzi unaendelea kulihusu. Atashtakiwa
mahakamani ikiwa atapatikana na hatia,” alisema.
Mkuu
huyo wa polisi aliomba maafisa wawe wakitafuta ushauri ili kuzuia matukio kama
hayo kushuhudiwa.
Credit Swahili hub
No comments:
Post a Comment