BAO
la Dakika ya 19 la Karim Benzema limewapa Real Madrid ushindi wa Bao 1-0 dhidi
ya Mabingwa Watetezi Bayern Munich kwenye Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali ya
UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI iliyochezwa Uwanja wa Santiago Bernabeu huko Madrid,
Spain usiku wa kuamkia leo.
Timu
hizi zitarudiana huko Allianz Arena, Jijini Munich Jumanne Aprili 29.
Wakati
Bayern wanawania kuwa Timu ya Kwanza kufanikiwa kutetea Taji lao, Real wanataka
kufuta uteja toka Bayern ambayo imeitoa katika Nusu Fainali 4 kati ya 5
walizokutana kwenye Mashindano haya ya Ulaya.
Jumanne
Usiku, kwenye Mechi nyingine ya Kwanza ya Nusu Fainali iliyochezwa huko Estadio
Vicente Calderon Jijini Madrid, Atletico Madrid na Chelsea zilitoka Sare ya
0-0.
Marudiano
Jumanne Aprili 29
Bayern
Munich v Real Madrid [0-1]
Jumatano Aprili 30
Chelsea
v Atletico Madrid [0-0]
FAINALI:
Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014
Bayern
Munich/Real Madrid v Chelsea/Atletico Madrid
No comments:
Post a Comment