WANAWAKE
WALIOBAKWA LIBYA KUFIDIWA
Waziri
wa Sheria nchini Libya ,salaha al-Marghani,amesema kuwa Baraza la mawaziri
limekubaliana kuwa Wanawake waliobakwa wakati wa maandamano na harakati za
kuuangusha utawala wa aliyekuwa Rais wa taifa hilo Moammar Gaddafi mwaka 2011
watambuliwe kuwa waathirika wa vita.
Amesema
makubaliano hayo yanayohitaji kuidhinishwa na Bunge kabla ya kuwa Sheria
yatamfanya mwanamke awe sawa na wale wapiganaji waasi waliojeruhiwa
halikadhalika watalipwa fidia.
Mahakama
ya kimataifa ya uhalifu imekusanya ushahidi kuwa vikosi vya waliokuwa
wakimuunga mkono Gaddafi walitekeleza vitendo vya ubakaji kama silaha.Inaelezwa kuwa Wanawake wanaobakwa mara nyingi wamekuwa wakitengwa nchini Libya, hivyo haijafahamika wanawake wangapi watajitokeza.
WANAOVAA NUSU UCHI KWENDA JELA MIAKA 10 HUKO NCHINI UGANDA
Rais wa
Uganda, Yoweri Museveni, ametia saini sheria mpya inayotoa adhabu kali kwa
watakaopatikana na hatia ya kutembea nusu uchi au kuhusika na vitendo
vinavyohusisha picha zenye watu uchi.
Wanawake
pia wamezuiwa kabisa kuvalia sketi fupi sana au ‘Mini Skirt’ kama
zinavyojulikana au blausi ambazo zinaonyesha kifua chao hadharani na
kusababisha hisia za kingono .Sheria hiyo inasema kuwa nguo kama hizo zitakubalika tu ikiwa zinatumika
kwa ajili ya mafunzo au wakati wa michezo na hafla za kitamaduni.
Akihutubia waandishi wa habari, mjini Kampala, waziri wa maadili na utawala bora, Reverend Simon Lokodo alisema kuwa Rais Museveni alipitisha sheria hiyo tarehe 6 mwezi huu, miezi mwili bada ya bunge kuipitisha.
Kwa mujibu wa sheria hiyo kamati dhidi ya vitendo hivyo itabuniwa ili iweze kutekeleza sheria hiyo kwa kuhakikisha kuwa picha, au video zenye watu uchi zinanaswa na kuharibiwa. Kamati hiyo, itajumuisha watu kutoka katika sekta mbali mbali ikiwemo ya habari na utumbuizaji.
Sheria hiyo inasema kuwa mtu yeyote atakayepatikana akijihusisha na vitendo vya watu kuwa uchi, kuvalia nusu uchi , kuona sinema za watu wakiwa uchi au kuchapisha picha za watu walio uchi kwa lengo la kuleta hisia tofauti utachukuliwa hatua kali za kisheria.
Waziri alisema kuwa serikali haitaki watu kuvalia nguo zisizo na heshima na kuzua hisia zisizofaa miongoni mwa watu. Watakaopatikana wakivunja sheria na kuvalia visivyo watafungwa hadi miaka 10 na wale watakaopatikana na hatia ya kuhusisha watoto katika biashara ya ngono watafungwa hadi miaka 15.
BBC
No comments:
Post a Comment