WAGANDA NA
TANZANIA WATIA FORA KATIKA KUSHEREHEKEA VALENTINE UKILINGANISHA NA KENYA
ULIMWENGU
mzima leo unaadhimisha Siku ya Wapendanao.
Utafiti
uliofanywa Kenya, Uganda na Tanzania na kampuni ya Ipsos Synovate unaonyesha ni
asilimia 65 pekee ya Wakenya waliohojiwa watakaosherehekea siku hii.
Hiyo
ni kinyume na wenzao wa Tanzania (69) na Uganda (71).
Na
hata kati ya hao watakaosherehekea, asilimia 23 wanasema hawatatumia zaidi ya
Sh1,000.
Mkurugenzi
Mkuu wa Ipsos Synovate, Bi Maggie Ireri, alisema hali hiyo inaibua maswali
kuhusu kinachowasukuma Wakenya kutokuwa na hamu ya kusherehekea siku hii ya
Velentino.
“Utafiti
huu umeibua swali kubwa - je Waganda na Watanzania wana mahaba zaidi ya
Wakenya? Ama ni gharama ya juu ya maisha inayoshuhudiwa Kenya ndiyo iliyoathiri
jinsi watakavyotumia pesa katika siku hii?”
Kwa
mfano asilimia 42 wanaotarajia zawadi za nguo ni kutoka Tazania. Uganda ni
asilimia 36 na Kenya ni asilimia 31.
Kwa
upande wa maua Waganda ni asilimia 37, Wakenya (36) na Watanzania (31).
Katika
kusherehekea siku hii, Watanzania wana matumaini makubwa zaidi kwamba itakuwa
iliyojaa mahaba kwa asilimia 72. Lakini Uganda na Kenya hawaamini hivyo.
Kiwango cha wanaokubaliana na wenzao wa Tanzania ni asilimia 56 nchini Uganda
na asilimia 52 pekee Kenya.
Hali
hiyo pia inajitokeza miongoni mwa wale ambao hawana nia ya kusherehekea siku
hii.
Utafiti
huu unaonyesha kuwa watakaokosa kushehekea kwa sababu ya gharama ya maisha
nchini Tanzania ni asilimia 58 wakifuatwa na Wakenya (asilimia 57) huku Waganda
wakiwa asilimia 43.
Utafiti
huu ulifanywa kati ya Februari 7 na 10 katika nchi za Kenya watu 1,050, Uganda
(1,006) na Tanzania (528) mtawalia.
No comments:
Post a Comment