HAPPY VALENTINE DAY
![]() |
I LOVE YOU VALENTINE WANGU |
Leo nimeona niongelee kidogo nini maana ya Valentine kwa asili yake
kisha kila mtu kwa Imani yake na mapana yake akatambua kuwa anapokuwa sehemu ya
Valentine Day anakuwa ana adhimisha nini maana wengi tunasheherekea Pasipo
kujua asili yake.
Inaonekana maana
halisi ya siku yenyewe inaharibiwa na watu wanaotumia fursa ya Valentine’s Day
kufanikisha matakwa ya misukumo ya tamaa za miili yao.
Siku ya leo nchi zote za duniani hua zinaadhimisha siku
hiyo ya wapendanao.
Ni wakati kama huu wa mwezi wa Februari ya kila mwaka
ambapo maua husambazwa, wapenzi hupeana kadi za mapenzi, hutumiana sms za
mahaba, kukiri makosa ya kimapenzi na kupeana miadi mipya ingawa haitekelezeki,
yote hayo kwa lengo ni kuimalisha mapenzi baina ya wapendanao katika ‘Siku ya
Wapendanao’ (Valentines’Day) Siku ya Februari 14.
Lakini , Jee tumeshawahi kujiuliza Valentine alikuwa nani
na wapi utamaduni huo wa siku ya Valentine umetoka na nini malengo ya sikukuu
hiyo?
HISTORIA YAKE FUPI
Historia yake imeanzia karne ya 3 huko Roma
ambapo alikuwapo padri Valentinus ambaye akaja kuheshimiwa kama mtakatifu hasa tarehe hiyo.
Inasemekana kwamba Kaisari wakati huo alikuwa Claudius II: yeye aliona kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule
asiyeoa wala kuwa na familia (kapera). Hivyo alipiga marufuku ndoa kwa
askari.
Valentinus alipinga
jambo hili hivyo kuendelea kufungisha ndoa kwa siri. Mfalme Claudius alipopata habari
hizi aliamuru Valentinus akamatwe na kuuawa.
Wakati akiwa gerezani vijana wengi walikwenda
kumtembelea, Valentinus aliandika barua ambayo ilikuwa na salamu za kwanza
za Valentine kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani; huyo
binti inasemekana alikuwa ni wa askari jela na mara nyingi alikuwa anamtembelea
kule gerezani.
Kabla anakwenda
kunyongwa akaacha ujumbe wa barua ambao mwisho wake alihitimisha kwa maneno haya: Kutoka
kwa Valentinus wako. (From your valentine)
Toka hapo Valentine
anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na sikukuu yake kuadhimishwa kote
duniani.
Aliyetangaza rasmi kuadhimisha siku hiyo ni Papa
Gelasius.
Kwa hiyo kwa kifupi siku hiii inawahusu waliopo kwenye
mapenzi hasa mwanamume na mwanamke.
Ingawa watu siku hizi wameichukulia kama ni kuonyesha
upendo kwa yeyote iwe baba, mama, kaka,
mjomba si vibaya llakini hiyo siyo maana yake halisi.
Lakini pia baadhi ya watu wameibadilisha maana ya siku
hii muhimu kwa wapendanao, na kuwa ni siku ya kufanya mambo yasiyofaa. Kwao,
wapendanao ni ngono. Kuna ambao huanzisha uhusiano siku hiyo kwa lengo la
kupata mtu wa kustarehe naye, hili ni kosa.
Kama mtazamo wako ni kutafuta mpenzi mpya na kwenda
kustarehe naye utakuwa unakosea sana. Haina maana ya ngono wala anasa na
kuharibu fedha kwenye ulevi. Yapo mengi ambayo unaweza kuyafanya kwa lengo la
kuifanya siku yako kuwa nzuri.
Kama unafikiri unao upendo kwa watu basi bora hizo pesa
ambazo ungezitumia kwa starehe basi nenda katoe msaada kwa wenye shida.
Katika jamii yetu kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wazee na wahitaji wengine. Tumia ulichojaliwa kushiriki nao utakuwa umeonesha namna unavyotambua umuhimu wa upendo.
Katika jamii yetu kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wazee na wahitaji wengine. Tumia ulichojaliwa kushiriki nao utakuwa umeonesha namna unavyotambua umuhimu wa upendo.
Ifanye siku hiyo kuwa ya tofauti zaidi kwa kudumisha
uhusiano wako na mpenzi wako na kuzungumzia changamoto mbalimbali za uhusiano
wenu kuliko kuwaza starehe na anasa ambazo hupoteza fedha.
Ondoa
fikra mbaya kichwani mwako rafiki, Waza kuhusu mema na kupendana kwa dhati,
hapo utakuwa umekwenda sawa na maana ya sikukuu yenyewe.
Nawatakia velentine day njema kwa wale wanaojua maana.
Nawatakia velentine day njema kwa wale wanaojua maana.
No comments:
Post a Comment