Monday, February 10, 2014

MCHUNGAJI AFUMANIWA NA MKEWE, MKE AMSEMEHE ASEMA YEYE NI KAMA MJESHI ALIYEJERUHIWA


Mchungaji mmoja aliyefumaniwa akiwa na mke wa mtu hotelini mjini Embu amesamehewa na mke na watoto wake. Mkewe alisema yeye ni kama mwanajeshi aliyejeruhiwa, na hawawezi kumtoroka mumewe.

Mchungaji huyo ameomba msamaha kwa kanisa lake na familia yake kwa yale aliyoyatenda.

Antony Maina wa kanisa la Kenya Assemblies of God (KAG) ambaye alikuwa ameandamana na familia yake alisema hakushiriki ngono na mwanamke waliopatikana pamoja katika hoteli moja mjini Karatina, Nyeri.

“Nataka kufafanua kuwa siko hapa kujitetea kwa yale yaliotokea. Niko hapa kujulisha kila mtu nchini kuwa nilifanya makosa na mtu yule  nimemkosea sana Mungu na tayari nishamuomba msamaha. Wanahabari walinisadia sana kwa sababu ningetenda dhambi nyingi zaidi. Kuja kwenu kulizuia kufanyika kwa mambo mabaya zaidi,” alisema Kasisi Maina.

Mkewe Beth Maina alisema familia imemsamehe na watasimama na yeye wakati huu anapokabiliwa na shutuma hizo.

“Bwanangu ni kama mwanajeshi aliyejeruhiwa katika makabiliano, wakati mwanajeshi anapopata majeraha wanajeshi wengine humsaidia bila kumuacha nyuma. Kanisa linapaswa kumsaidia pia katika suala hili,” alisema Bi Maina.

Kasisi Maina ambaye pia alikuwa ameandamana na wanawe wawili aliyesema shughuli za kanisa hilo zitaendelea tu kama kawaida.

Makasisi wa kanisa hilo walisema Bw Maina kwa sasa amesimamishwa kazi huku uchunguzi ukiendelea kulingana na kanuni na mafunzo ya dhehebu hilo.
Credit Swahili hub

No comments: