Wednesday, February 19, 2014

UEFA CHAMPIONZ LIGI UCL: BARCA YAIPIGA CITY 2-0 ETIHAD, PSG YAINYUKA 4-0 LEVERKUSEN

UEFA CHAMPIONZ LIGI, imeendelea usiku wa kuamkia leo kwa Timu za Nyumbani zote kutandikwa wakati Barcelonawalipoiwasha Manchester City 2-0 huko Etihad na Paris Saint-Germain kuitandika Bayer Leverkusen Bao 4-0 huko Bay Arena, Jijini Leverkusen, Ujerumani, hizo zikiwa Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16.

MANCHESTER CITY 0 BARCELONA 2
PENATI ya Dakika ya 54 ya Lionel Messi iliwafungulia njia Barcelona na kupata ushindi wa Bao 2-0 walipocheza na Manchester City Uwanjani Etihad katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Penati hiyo ilitolewa baada ya Demichelis kumwangusha Messi aliekuwa anaenda kukutana na Kipa Joe Hart na pia kusababisha Beki huyo wa Man City kupewa Kadi Nyekundu na Refa Jonas Eriksson kutoka Sweden.
Barcelona walifunga Bao lao la Pili katika Dakika ya 90 kupitia Dani Alves baada ya kazi nzuri ya Neymar alieingia Kipindi cha Pili.
Timu hizi zitarudiana huko Nou Camp hapo Machi 12 na City watahitaji kushinda Bao 3-0 ili wasonge Robo Fainali.

BAYER LEVERKUSEN  0 PARIS SAINT-GERMAIN 4

Wakicheza kwao BayArena Jijini Lerkusen, Nchini Germany, Bayer Leverkusen wametandikwa Bao 4-0 na Paris Saint-Germain ambao hadi Mapumziko walikuwa mbele kwa Bao 3-0.
Bao za PSG zilifungwa na Blaise Matuidi, Dakika ya 3, na mbili za Zlatan Ibrahimovic, kwenye Dakika ya 39 kwa Penati na jingine kwa mzinga mkali nje ya Boksi katika Dakika ya 42 huku Bao la 4 likipachikwa na Yohan Cabaye kwenye Dakika ya 88.
Kuanzia Dakika ya 59, Leverkusen walicheza Mtu 10 baada ya Emir Spahic kupewa Kadi Nyekundu kufuatia Kadi za Njano mbili.


Leo Jumatano Februari 19

22:45 AC Milan v Atletico de Madrid

22:45 Arsenal FC v Bayern Munich

No comments: