MWANAMKE AUAWA
NA MUMEWE BAADA YA KUFUMANIWA AKIZINI NA BINAMU YAKE MBEYA
![]() |
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ahmed Msangi |
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ahmed Msangi, alisema mwanamke huyo aliuawa juzi majira ya saa 11:00 jioni nyumbani kwake katika Kijiji cha Inyara.
Alisema tukio hilo la kinyama linadaiwa kufanywa na mume wa marehemu, Ezekiel Mwakabenga (21) ambaye anadaiwa kumpiga mkewe kwa kutumia ngumi, fimbo na mateke na kumsababishia majeraha makubwa ambapo alikimbizwa katika hospitali ya rufaa jijini humo na kufariki dunia akiwa anapata matibabu.
Msangi alisema Mwakabenga ambaye ni mfanyabiashara alimkuta mkewe akifanya mapenzi na binamu yake ndani ya nyumba yao, kitendo ambacho kilimchukiza, hivyo kuamua kumpiga.
Mwilii wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya na mtuhumiwa anashikiliwa na polisi.
No comments:
Post a Comment