Thursday, November 7, 2013

AARON RAMSEY AWALIZA WAJERUMANI PALE ARSENAL ILIPOIKANDAMIZA  BORUSSIA DORTMUND 1-0
ETO'O NAYE APELEKA KILIO KWA  WAJERUMANI WENGINE APIGA MBILI CHELSEA IKIUA SCHALKE 04.
MESSI NAYE , AIPIGIA MBILI BARCA NA KUINYONGA AC MILAN ULAYA
Aaron Ramsey akifunga bao
BAO pekee la Aaron Ramsey dakika ya 62, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya wenyeji Borussia Dortmund nchini Ujerumani.

Hilo linakuwa bao la 13 kwa mchezaji huyo msimu huu na bao la tano katika michuano ya Ulaya msimu huu. Pamoja na kufungwa, wenyeji ndio waliocheza vyema usiku  wa kuamkia leo kabla ya Arsenal kupata bao lake, hawakuweza kutengeneza nafasi hata moja ya kufunga.
Borussia ambayo inapewa sifa ya moja ya timu bora kabisa Ulaya kwa sasa, iliingia kwenye mechi hiyo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 6-1 dhidi ya Stuttgart katika ligi ya kwao, Bundesliga, lakini ilikalishwa na mtutu mmoja wa bunduki.
Katika mechi nyingine, Barcelona imeifunga AC Milan mabao 3-1 Uwanja wa Camp Nou, Lionel Messi akifunga mawili dakika ya 30 na 83, wakati lingine limefungwa na Busquets dakika ya 40, huku Pique akijifunga dakika ya 45 kuwapatia wageni bao la kufutia machozi.
Nayo Chelsea imeifumua 3-0 Schalke 04, mabao ya Samuel Eto'o dakika ya 31 na 54 na Demba Ba dakika ya 83.
Matokeo mengine
Ajax
Celtic 
Basel
Steaua Bucuresti

SSC Napoli
Marseille

Zenit Petersburg
FC Porto

Atletico Madrid
Austria Wien  





No comments: