Wednesday, November 6, 2013

HAYA SASA MAKUBWA, ASKOFU ADAIWA TALAKA NA MKEWE
Dk Jacob Erasto Chimeledya kiongozi Anglikana Tanzania
Askofu wa kanisa la Anglikana Doyosisi ya Rorya John Adiema,amefunguliwa  mashitaka ya madai na mke wake wa ndoa ambapo pamoja na mambo mengine mwanake huyo ameimbiama hakama ya hakimu mkazi mkoa wa Mara kutengua ndoa yao na kupewa  talaka. 

Kesi hiyo namba moja ya mwaka huu ambayo  inatajwa kuwa ya kwanza kutokea  kwa kanisa hilo nchini,ikihusu askofu kufikishwa mahakamani imepangwa kusikilizwa
Novemba 18 mwaka huu katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Mara mjini Musoma.

Mke wa kiongozi  wa mkuu wa kanisa la Angilikana Dayosisi ya
Rorya Bi Peres Adiema,akizungumza baada ya kufungua shauri hilo mahakamani hapo,amesema pamoja na talaka pia anamdai mume  wake huyo haki zake zote za msingi walizochuma wakiwa kama wana ndoa.
Lukwangule blog

No comments: