Wednesday, October 9, 2013

FIFA YAANZISHA MTANDAO WA UHAMISHO NDANI YA NCHI (DTMS), GHANA YAITAKA FIFA KUONDOA MECHI NCHINI MISRI
LEO FIFA inazindua Mtandao wa Domestic Transfer Matching System (DTMS) ili kuzisaidia Mchi Wanachama wake kuendesha Uhamisho wa Wachezaji ndani ya Nchi zao.
DTMS unachukua muundo wa ITMS (International Transfer Matching System) ambao umekuwa ukimudu Uhamisho wa Kimataifa wa Wachezaji na hii DTMS itagawiwa kwa Nchi Wanachama zaidi ya 200 na Klabu 6,500.
DTMS na ITMS zinaingiliana na zinapatika katika sehemu moja ya Mtandao.
FIFA imesema DTMS itazidisha udhiti wa Uhamisho wa Wachezaji kwa kuwepo uwazi wa kuzingatia Kanuni za Uhamisho.
Pia Mtandao huo utarahisisha Malipo ya Uhamisho na kuondoa utata uliokuwepo hivi sasa wa Klabu kurushana Fedha katika Uhamisho.
FIFA imesema moja ya faida kubwa ya kutumia DTMS ni kufanya Uhamisho wa Wachezaji uwe mwepesi na wa haraka kukamilisha huku kumbukumbu zake zikiwa rahisi kuhifadhiwa.
DTMS inatarajiwa kuanza rasmi kutumika na Nchi Wanachama wa FIFA Mwakani.
GHANA YAITAKA FIFA KUIONDOA MECHI NCHINI EGYPT
GHANA wameitaka FIFA kuitazama upya Mechi yao na Egypt ya kuwania kwenda Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia Mwakani iliyopangwa kuchezwa Mjini Cairo hapo Novemba 19 ili ihamishwe toka Nchini Egypt kwa vile hali ya usalama inatisha.
Chama cha Soka cha Ghana, GFA, kimeiandikia FIFA kuitaka kutazama hali ya usalama Nchini humo na kuangalia upya Mechi hiyo kuchezwa Mjini Cairo.
Ghana imeitaka FIFA kutazama uamuzi wa Misri kuiweka Mechi hiyo Mjini Cairo na kuchezwa mbele ya Watazamaji kitu ambacho hakijafanyika Nchini humo kwa Miaka miwili ambapo Watazamaji wamekuwa hawaruhusiwi kuingia kwenye Mechi kwa sababu za kusalama.
Egypt ilizuia Watazamaji kuingia kwenye Mechi baada ya Vifo vya Watu 74 kwenye Uwanja Mjini Port Said lakini kwa Mechi za Timu ya Taifa, Watazamaji wachache wamekuwa wakiruhusiwa.
Kwa sasa huko Egypt Mechi zote zimesimama isipokuwa zile za Timu ya Taifa na Klabu mbili tu, Al Ahli na Zamalek, zilipokuwa zikicheza michuano ya CAF CHAMPIONZ LIGI na Mechi zote hizo zimekuwa zikichezwa Mji mdogo wa El Gouna uliopo kando kando ya Red Sea na bila ya Watazamaji kuwepo.
Lakini kwa Mechi hiyo ya Ghana na Egypt hapo Novemba 19, ambayo itakuwa ni ya Marudiano baada ya kucheza huko Kumasi, Ghana hapo Oktoba 15, imeamuliwa kuchezwa Mjini Cairo mbele ya Mashabiki wao ili kuipa nafasi Egypt iweze kucheza Fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu Mwaka 1990.

No comments: