MBUNGE NCHINI KENYA AWAZAWADIA WANAWAKE 16 KWA KUJIFUNGUA WATOTO
![]() |
Mimba |
WANAWAKE
16 katika eneo la Kirinyaga huko nchini kenya wametuzwa na mbunge wao wa
Gichugu Bw Ejidio Njogu Barua baada ya kujifungua watoto.
Mbunge
huyo aliwasifu wanawake hao kwa kutilia mkazo wito wake kuwa waimarishe juhudi
zao za kuongeza kizazi katika maeneo hayo na akaahidi kuendelea mbele na mradi
huo.
Katika
hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Kanisa la Katoliki Mururi katika eneo la bunge
hilo mnamo Ijumaa, kila mwanamke alipokea Sh500, wote wakipata jumla ya Sh 8,000.
“Nilikuwa
nimepata habari za kufurahisha kuwa ni wanawake 48 ambao walikuwa wajitokeze
mahali hapa. Nilikuwa nimebeba Sh24,000 lakini nimeshangaa kupata wanawake 16
pekee. Lakini silalamiki sana kwa kuwa hii ni idadi nzuri ikizingatiwa kuna
miezi kadhaa ambayo haungemuona mja mzito barabara za eneo hili letu,” akasema.
Bw
Barua alisema kuwa atazidisha kampeni yake miongoni mwa vijana ambao wamekwama
katika unywaji wa pombe kiholela na kisha kusahau majukumu yao ya kijamii
warekebike na kisha waanzishe familia zao.
“Mimi
nataka kuwatangazia kwamba juhudi hizi zitakuwa zikiendelea kila wikiendi
ambapo ukishapata mimba na kisha ujifungue mtoto, nitakutuza
Sh500
kama zawadi. Kisha tufuatilie juhudi hizo kwa kuhakikisha umejiunga na kikundi
cha ustawi na upate hela za kujiendeleza kiriziki,” akasema.
Mradi
huo ni sawia na mwingine unaoendeshwa na Gavana wa Kaunti hiyo Bw Joseph Ndathi
ambaye pia huwatuza kina mama waliojifungua baada ya kuolewa na vijana ambao
wamehepa ulevi.
Aliwahimiza
viongozi wa kanisa wazindue maombi maalum ili vijana wa eneo hilo watilie mkazo
uzazi.
Mbunge
huyo alisema hali ya sasa kwa vijana ni kulewa pombe haramu na kisha kujisahau
kifamilia.
“Hatutaki kujiona kwa vyombo vya habari
tukitangaziwa kwa wanawake wetu wanaandamana wakiwalaumu waume zao wakibugia
pombe hatari,”akasema.
Mbunge
huyo aliwachangamsha aliposema kuwa alikuwa akihofia kama atafanikiwa
kuchaguliwa tena 2017 ikiwa vijana wa eneo hilo watasombwa na ulevi jinsi
ilivyo kwa sasa na kisha kuaga dunia.
Alisema
kuwa amekuwa akizuru hospitali ya Kianyaga na kuthibitisha kuwa wadi za
kujifungulia wamama zimefanywa stoo za kuweka vifaa.
"Hii
ni kwa sababu madaktari wamechoka kungoja waja wazito. Ni nadra sana wapate
wanawake vijana wakiletwa humo wakiwa waja wazito,".
Bwana
Barua alisema kuwa, kungekuwa na uwezekano wa kuunda sheria ya kuwashinikiza
vijana waunde familia kwa lazima, angewasilisha mswada bungeni.
Aliomba
waumini wajifunge kula na kunywa ili wamuombe Maulana kuwaokoa vijana. Aliapa
kuwasukuma maafisa wa utawala kupambana na wagema wa pombe haramu.
Aidha,
aliwataka wenyeji kuwashinikiza vijana wauteme ulevi na kisha waoe.
"Hata
ikiwa itahitaji tuwahonge vijana hao ndio warekebike, tutawahonga,"
akasema.
Swahili hub
No comments:
Post a Comment