MCHEZO WA NGUMI WAFANA IDD MOSI MJINI MTWARA IDEFONCE MNALI WA BLACK MAMBA MTWARA AMCHAKAZA SHAHA KASIMU WA MZIMUNI DSM
 |
Mabondia kutoka club za black Mamba ya mtwara na Mzimuni wa Dsm wakisubiri kukaguliwa na mgeni rami kamanda wa police mkoani mtr Linus Sinzumwa. |
 |
Burudani haikuwa nyuma Mtwara Dancers wakifanya vitu vyao |
 |
Wamuzi kamishna Kulwa Makaranga Kushoto na Riadha Kimweri katikati wakiwa na Daktari wa mchezo |
 |
Meneja wa Black Mamba Mahamudu Sinani akiwatambulisha wageni |
 |
Mgeni rasmi Kamanda wa polisi mkoani Mtwara Linusi Sinzumwa akijiandaa kusoma hotuba |
t |
Kamanda Sinzumwa kiwatakiwa wachezaji mchezo mwema na wa amani |
 |
Ndonga zimeanza Abdalah na Taliki |
 |
Ashrafu na Selemani |
 |
Shongo akienda chini baada ya makonde mazito toka kwa Mwl Musa |
|
 |
Mwl Musa (teache alone) akifa nya vitu vyake dhidi ya Shongo | | | |
|
|
|
|
 |
Idefonce Mnali na Shaha Kasimu |
Bondia anayechipukia mkoani mtwara Idefonce Mnali kutoka
katika club ya Black Mamba jana usiku wa
ameweza kumchakaza bondia Shaha Kasimu katoka katika club ya Mzimuni Mogomeni
DSM katika mchezo usio na ubingwa wa uzito wa Super Middle uliopigwa katika dimba
la Nangwanda sijaona mjini Mtwara sikuku ya Idd Mosi.
Mchezo huo ambao ulikuwa wa round sita, Idefonce aliweza kumchakaza Shaha kwa point 58 kwa 56.
Katika Mpambano huo ambao Mgeni rasmi alikuwa kamanda
wa police Mkoani Mtwara, Linus Sinzumwa
ulitanguliwa na mapambano manne ya
utangulizi.
Pambano la kwanza liliwakutanisha watoto Abdalh Ashrafu
na Taliki maafudhi na Abdalah Ashraf kuibuka kidedea kwa point 30 kwa 27.
Mpambano uliofuata ulikuwa ni kati ya Ashrafu Abdalah wa
Black Mamba na Seleman Shabani wa Mzimuni katika uzito wa Fly Weight Raound nne
na hatimaye wababe hao kwenda sare kwa kufungana point.
Mpambano mwingine wa kuvutia wa uzito wa Light Welter
Weight ulikuwa ni kati ya Muhamedi Ahamad (Penta boy) wa balack Mamba na Bahati
kalembo wa Mzimuni ambapo Bahati aliweza
kumshinda Penta Boy kwa point 39 kwa 38.
Na mpambano wingine ulikuwa ni kati ya Mwalimu
Musa wa Mzimuni na Shongo Ally wa Black
Mamba, ambapo Shongo alitandikwa kwa Knock Out round ya pili ambapo alikenda
chini mara mbili na kushindwa kuendelea na mchezo.
Mapambano yote yalichezeshwa na kamishna wa ngumi wa
kimataifa wa IBF, TBC na AUB Kulwa Makaranga akisaidiwa na Riadha Kimweli.
No comments:
Post a Comment