AUWAWA NA KUCHOMWA MOTO BAADA YA MPENZI WAKE KUMPIGIA KELELE ZA MWIZI
![]() |
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari |
Mwanamke mmoja mkazi wa Magazini mjini Mpanda
mkoani Katavi amesababisha kifo cha
mpenzi wake baada ya kumuitia mwizi, na kisha kuvamiwa na watu waliompiga na
kumchoma moto hadi kufa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, amethibitisha kuuawa kwa mkazi huyo Florence Mabuga (29), katika kisa hicho kilichotokea katika mtaa wa Nsemulwa-Magazini hivi karibini, usiku wakati Mabuga akimsindikiza mpenzi wake wa kike akitokea nyumbani kwake.
Akisimulia mkasa huo wa kusikitisha, Kamanda Kidavashari alisema Mabuga ambaye alikuwa msimamizi wa vibarua wa kujenga nyumba mjini humo, siku hiyo baada ya kurejea nyumbani, alitembelewa na mpenzi huyo ambaye jina lake halijafahamika.
Inadaiwa wakati Mabuga akimsindikiza rafiki huyo, ulizuka mzozo baina yao ambapo Mabuga alitishia kuwa usiku huo angechoma nyumba ya rafiki huyo, ndipo kwa hasira na hofu ya kuchomewa nyumba, alipiga yowe akiashiria kuwa Mabuga ni mwizi.
Kwa mujibu wa Kidavashari, Mabuga alianza kutimua mbio mara alipoona kundi la wananachi wenye hasira wakiwa na silaha mbalimbali za jadi wakikimbilia alipokuwa amesimama na rafiki yake huyo.
Inadaiwa kuwa wananchi hao walifanikiwa kumkamata Mabuga aliyekuwa akijaribu kuingia ndani ya nyumba yake, na kuanza kumpiga na kumsababishia mauti.
“Uchunguzi wa awali wa kipolisi umebaini kuwa Mabuga alisingiziwa tu na mpenzi wake huyo, kwani hakuiba kitu chochote, ila mpenzi wake huyo alimpigia mayowe ya mwizi baada ya kuzuka mzozo baina yao,“ alidai.
Kwa mujibu wa Kidavashari mtuhumiwa huyo anaendelea kusakwa ili sheria ichukua mkondo wake, pia hakuna mtu yeyote aliyekamatwa hadi sasa kwani wananchi hao walikimbia eneo la tukio mara baada ya kufanya unyama huo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, amethibitisha kuuawa kwa mkazi huyo Florence Mabuga (29), katika kisa hicho kilichotokea katika mtaa wa Nsemulwa-Magazini hivi karibini, usiku wakati Mabuga akimsindikiza mpenzi wake wa kike akitokea nyumbani kwake.
Akisimulia mkasa huo wa kusikitisha, Kamanda Kidavashari alisema Mabuga ambaye alikuwa msimamizi wa vibarua wa kujenga nyumba mjini humo, siku hiyo baada ya kurejea nyumbani, alitembelewa na mpenzi huyo ambaye jina lake halijafahamika.
Inadaiwa wakati Mabuga akimsindikiza rafiki huyo, ulizuka mzozo baina yao ambapo Mabuga alitishia kuwa usiku huo angechoma nyumba ya rafiki huyo, ndipo kwa hasira na hofu ya kuchomewa nyumba, alipiga yowe akiashiria kuwa Mabuga ni mwizi.
Kwa mujibu wa Kidavashari, Mabuga alianza kutimua mbio mara alipoona kundi la wananachi wenye hasira wakiwa na silaha mbalimbali za jadi wakikimbilia alipokuwa amesimama na rafiki yake huyo.
Inadaiwa kuwa wananchi hao walifanikiwa kumkamata Mabuga aliyekuwa akijaribu kuingia ndani ya nyumba yake, na kuanza kumpiga na kumsababishia mauti.
“Uchunguzi wa awali wa kipolisi umebaini kuwa Mabuga alisingiziwa tu na mpenzi wake huyo, kwani hakuiba kitu chochote, ila mpenzi wake huyo alimpigia mayowe ya mwizi baada ya kuzuka mzozo baina yao,“ alidai.
Kwa mujibu wa Kidavashari mtuhumiwa huyo anaendelea kusakwa ili sheria ichukua mkondo wake, pia hakuna mtu yeyote aliyekamatwa hadi sasa kwani wananchi hao walikimbia eneo la tukio mara baada ya kufanya unyama huo.
No comments:
Post a Comment