MWANAMKE ATEKETEZA NYUMBA KWA MOTO BAADA YA MUME KUOA MKE WA PILI
![]() |
Mji wa Migori |
Baada
ya mwanamume mmoja kutoka mji wa Migori nchini Kenya kumuoa mke wa pili
mwishoni mwa wiki ilimsababishia hasara ya mamilioni baada ya mke wa kwanza
kukasirika na kuteketeza nyumba yake.
Mkewe
aliyejawa na hasira alirushia nyumba hiyo bomu la petroli katika kijiji cha
Nyakona, Got Kachola, eneo bunge la Nyatike kupinga ndoa hiyo.
Mali
zote zilizokuwa katika nyumba hiyo ikiwa ni pamoja na nguo, samani na vyombo
vya elektroniki vya thamani ya Sh1 milioni alivyomiliki Bw Simeon Osewe,
viliteketea kabisa.
Mkewe
wa kwanza, aliye mama wa watoto wawili aliwasili kwa siri kutoka Nairobi
anakofanya kazi na kumshambulia mke mwenza aliyekuwa akilala katika nyumba
hiyo.
“Nilikuwa
mjini Migori kwa shughuli za kibinafsi nilipopigiwa simu nikiarifiwa kwamba
nyumba yangu ilikuwa ikichomeka. Mke wangu wa pili alifanikiwa kutoroka na
kumwacha mke wa kwanza aliyechoma nyumba hiyo,” akasema Bw Osewe.
Juhudi
za wanakijiji kuzima moto huo hazikufaulu na moto mkali ukateketeza nyumba hiyo
hadi kila kitu kikawa jivu.
Mkuu
wa polisi wa Nyatike Bw Richard Mukwate alisema mwanamke huyo alikamatwa
akijaribu kutoroka eneo la mkasa.
Alisema
mwamamke huyo alionekana kukasirishwa na hatua ya mumewe kuoa mke wa pili na
kuishi katika nyumba hiyo.
“Tumemzuia
katika kituo cha polisi cha Macalder na tutamfikisha mahakamani wiki hii na
kumfungulia mashtaka ya kuchoma mali,” akasema Bw Mukwate.
Bw
Osewe alisema aliamua kuoa mke wa pili baada ya mke wa kwanza kukataa kuishi
naye mashambani.
“Mwanamke
huyo alikataa wito wangu wa kuja nyumbani akisema anapenda mazingira ya Nairobi
na hii ikanifanya kuoa kwa sababu sikuweza kuishi peke yangu mashambani,”
akasema.
Swahili
hub
No comments:
Post a Comment