AFUNGWA MIAKA 14 JELA KWA KUZINI NA MBUZI
![]() |
Picha kwa hisani ya Joachimjunior blog lakini haihusiani na tukio |
MWANAMUME
aliyepatikana na hatia ya kushiriki ngono na mbuzi amehukumiwa kifungo cha
miaka 14 jela na mahakama Taita Taveta.
James
Mbithe alishtakiwa kuwa mnamo Julai 9 katika kijiji cha Mgeno alifanya mapenzi
na mbuzi anayemilikiwa na Bi Hannah Mambori.
Upande
wa mashtaka ukiongozwa na Inspekta Peter Milimo ulisema mshukiwa alifumaniwa na
mlalamishi aliyekuwa ameenda kuwaangalia mbuzi wake 12 waliokuwa machungani
mita 300 kutoka nyumbani kwake.
Alimpata
mshukiwa aliyemfahamu vyema akiwa amevua suruali ndefu yake huku mbuzi akitokwa
na damu.
Baadaye
aliripoti kisa hicho kwa mzee wa kijiji na baadaye kwa afisa wa matibabu ya
mifugo ambaye alithibitisha kwamba mnyama huyo alikuwa amechafuliwa.
Mshtakiwa
anadaiwa kumtendea mbuzi huyo kitendo hicho mchana kama adhabu baada ya kuingia
shamba lake la mahindi na kuharibu mimea.
Mshtakiwa
alikiri kosa hilo akisema hangeweza kukanusha kwa kuwa ulikuwa ndio ukweli.
Akijitetea,
Mbithe, 59, aliomba ahurumiwe akisema ni mzee na kwamba alihadaiwa na shetani.
Akitoa
hukumu, Kaimu Hakimu Mkuu Wundanyi Bi M. Chesang alisema kwa kuzingatia
kujitetea kwa mshtakiwa, ripoti ya hali ya kiakili kutoka kwa Afisi ya
Uchunguzi wa Hali za Kiakili, na sheria, mshtakiwa anafaa kutumikia kifungo cha
miaka 14 jela.
Hukumu
hiyo imetolewa chini ya wiki moja baada ya Idara ya Mahakama ndogo ya Taita
kuzindua kampeni dhidi ya dhuluma za kimapenzi.
Hii
ni baada ya polisi kusema asilimia 12 ya visa vya uhalifu vilivyoripotiwa
kutoka eneo hilo kipindi cha miezi mitatu ni za dhuluma za kimapenzi.
No comments:
Post a Comment