OMBAOMBA ANAYETAPELI WATU KWA KUIGIZA HANA MKONO MMOJA NA MGUU ACHEZEA
KICHAPO AONYESHA MIKONO YOTE NA MIGUU, MPENZI WAKE ALIYEMTELEKEZA
NDIYE ALIYETOA SIRI
Akiwa kazini |
Akitimua mbio baada kukurupushwa siku za nyuma |
Akiwa amedakwa na wananchi wenye hasira leo |
Kichapo kinaanza |
Akishushiwa kipigo kitakatifu |
Tapeli
huyo mbali ya kuumbuliwa kwa kutakiwa kuonyesha
miguu yake yote pamoja na mikono yake yote bado
amepata kuchezea kichapo kiasi cha kunusurika
kuuwawa na wananchi hao wenye hasira kali.
Kutokana
na kufichuliwa kwa siri hiyo ya kujiigiza kuwa ni
omba omba mlemavu wananchi wamekuwa wakimtimua kila kona anayokaa tapeli
huyo na kumtimua mbio kabla ya leo wananchi hao kuamua
kumkimbiza kutoka eneo la Hazina Ndogo hadi miyomboni na kuanza
kumpa kichapo hadi alipoamua kuonyesha viungo vyote kuwa si
mlemavu
Tapeli
huyo mbali ya kujifanya ni mlemavu wa viungo wakati
mwingine huwa anajifanya ni mtu asiyeongea (bubu) asiye na viungo
kama mikono na miguu ila wakati mwingine akijifanya ni hana mguu
mmoja na kuwaomba watu fedha za matibabu .
Hata
hivyo baada ya mmoja kati ya wananchi kufika eneo hilo alionyesha kufichua
mbinu hiyo chafu ya mzee huyo kujifanya ni mlemavu wakati asubuhi alikutana
maeneo akiwa mzima wa afya njema na katika kumhoji zaidi ndipo kamera ya mtandao
huu ilipoamua kufanya kazi yake ya kunasa kituko hicho na ndipo mzee huyo
alipoanza kuongea kwa sauti vizuri tofauti na alivyokuwa akijifanya kuwa hawezi
kuongea kabisa (bubu)
Wakati
mabishano yakiendelea eneo hilo ghafla mzee huyo alisimama kwa miguu yake yote
miwili pamoja na awali kujifanya ni mlemavu asiye na mguu mmoja ila baada ya
watu kutaka apigwe picha ndipo mzee huyo alipoanza kutimua mbio huku ulemavu
aliokuwa nao akiusahau hapo kutokana na kichapo alichokipata
na kuumizwa vibaya usoni .
Hata
hivyo inasemekana mzee huyo amekuwa akiadhibiwa katika
maeneo mbali mbali kutokana na mbinu yake ya kufuru
anayoifanya kuwa ni mlemavu wakati si mlemavu na kuwa ni heri
kuomba kama mtu mwenye matatizo ya kiuchumi kuliko kuwaigiza
walemavu na kuwa iwapo atarudia na kukutwa akifanya hivyo
watamvunja kweli mkono ili kuwa mlemavu walisema wananchi hao.
Aidha
anadaiwa chanzo cha kichapo cha leo kwa mzee huyo
tapeli ni mmoja kati ya mpenzi wake ambae alikuwa amemsusa
na kuhamia kwa mpenzi mwingine kuueleza umma kuwa huyo ni
tapeli na yeye ni mpenzi wake ambae anamtambua kuwa na miguu yote,mikono
na si bubu kama anavyoigiza jambo lililopelekea wananchi kufanya
udadisi .
Kabla
kufukuzwa na kuchezea kichapo tapeli huyo alifukuzwa eneo ambalo
alikuwa amekaa barabara eneo la Santona na kutoka kuondoka haraka na mmoja kati
ya vijana wanaofanya kazi ya kusafisha na kushona viatu na
kupuuza na ndipo mtiti ulipoanza.
Baadhi
ya wananchi wameuomba uongozi wa Manispaa ya Iringa kuwabana omba omba hao
ambao wamekuwa wakidanganya watu kuwa wao ni walemavu kumbe ni wazima na kutaka
kuwepo kwa utaratibu maalum wa watu kuomba misaada.
No comments:
Post a Comment