JAMAA AMUA KUFUNGA NDOA NA MPENZI WAKE ALIYE KUFA ILI
KUTIMIZA AHADI YAKE.
![]() |
| Deffy akimvisha pete Kamsook |
![]() |
| Hapa akimpusu mchumba wake marehemu |
Mtu mmoja
huko nchini Thailand hivi karibuni ameamua kumuoa mpenzi wake aliyekufa lengo
ni kutimiza ahadi yao waliyojiwekea ya kuoana siku za usoni.
Chadil Deffy alimvisha
pete ya ndoa mchumba wake Anne Kamsook katika siku ya mazishi ambayo pia
ilikuwa siku ya sherehe ya harusi hiyo.
Deffy na
Kamsook waliwekeana ahadi ya kuoana siku za usoni lakini kwa bahati mbaya
Kamsook alikufa kwa ajali kwa bla ya
kutimiza adhima yao ya kuoana.
Deffy alihisi
hatakuwa amemtendea vema mchumba wake kutengana bila kufunga ndoa ndipo
alipoamua kuchukua maamuzi hayo.
Mbele ya
ndugu, jamaa na marafiki Deffy alimvisha
pete mchumba wake marehemu na kuhaidi kumpenda maisha yake yote.
Kamsook alizikwa
baada ya sherehe kumalizika.


No comments:
Post a Comment