TANZANIA YAPANDA KWA NAFASI NANE KATIKA VIWANGO VYA FIFA

SHIRIKISHO la Soka
Dunia-FIFA limetoa viwango vipya vya ubora katika soka kwa mwezi huu
ambapo Tanzania imekwea kwa nafasi nane mpaka katika nafasi ya 119
kwenye viwango hivyo. Mwezi
uliopita Tanzania ilikuwa katika nafasi ya 127 baada ya kuporomoka kwa
nafasi tatu ukilinganisha na viwango vya mwezi Januari ambapo ilikuwa
katika nafasi ya 124 baada ya kupanda kwa nafasi sita. Kwa
upande wa nchi zinazoshika tano bora duniani kwenye orodha hizo zote
zimeendelea kubakia katika nafasi zao ambapo Hispania imeendelea
kuongoza ikifuatiwa na Ujerumani katika nafasi ya pili huku katika
nafasi ya tatu ikishikwa Argentina wakati Uingereza na Italia zinashika
nafasi ya nne na tano. Kwa
upande Afrika Ivory Coast wameendelea kung’ang’ania katika nafasi ya
kwanza baada ya kuporomoka kwa nafasi moja mpaka ya 13 duniani
wakifuatiwa na Ghana ambao wako katika nafasi ya 20 huku Mali nao wakiwa
hawako mbali baada ya kupanda nafasi moja mpaka ya 24. Mabingwa
wa Afrika Nigeria wao wako katika nafasi ya nne kwa upande wa Afrika
baada ya kubakia katika nafasi yao ya 30 kama ilivyokuwa mwezi uliopita
kwenye orodha za dunia huku tano bora kwa upande Afrika ikifungwa na
Algeria.
No comments:
Post a Comment