Thursday, January 29, 2015

KUNDI D la Mashindano ya Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, limemaliza Mechi zao za mwisho kwa Ivory Coast kutinga Robo Fainali baada ya kuifunga Cameroun lakini Mali na Guinea zinangoja kurushwa Shilingi kuamua nani ataungana nao baada ya Timu hizo kutoka Sare kwenye Mechi yao ya mwisho na kufungana kwa kila kitu.
Ivory Coast wametinga Robo Fainali baada ya kuifunga Cameroun Bao 1-0 na kutwaa uongozi wa Kundi D katika dimba la  Nuevo Estadio de Malabo, Mjini Malabo.
Ivory Coast walitinga Haftaimu wakiwa Bao 1-0 mbele kwa Bao la Dakika ya 36 la Max-Alain Gradel kwa Shuti la Mita 30.
Na katika dimba la Estadio de Mongomo, Mjini Mongomo, Guinea walitangulia kupata Bao lao kwa Penati iliyotolewa Dakika ya 13 kufuatia Wague kuunawa Mpira na Kevin Constant kufunga Penati hiyo.
Mali walishindwa kusawazisha Dakika chache baadae baada ya wao pia kupewa Penati kufuatia Issiaga Sylla kuunawa lakini Seydou Keita alipiga Penati dhaifu iliyookolewa na Kipa Naby Yattara, Hadi Mapumziko Guinea 1 Mali 0.
Kipindi cha Pili Modibo Maiga, Mchezaji wa West Ham anacheza kwa Mkopo Metz ya France, aliawazisha kwa Mali kwa Kichwa baada ya Krosi ya Abdoulay Diaby.
Timu zote mbili Guinea na Mali zote zina pointi sawa na magoli matatu ya kufunga.
Kwa sasa timu moja kati ya Guinea au Mali itasonga mbele hatua ya robo fainali baada ya kura itakayopigwa hii leo na Shirikisho la Soka barani Afrika CAF.

No comments: