Tuesday, December 24, 2013

AMCHARANGA MAPANGA NA KUMKATA MKONO MCHUMBA WAKE KWA WIVU WA KIMAPENZI

Huko Wilayani Liwale Mkoani Lindi, Mkazi Mmoja wa kijiji cha Naluleo aliefahamika kwa Jina la Shida Mapele amejeruhiwa vibaya kwa Mapanga na Mchumba wake na kumsababishia ulemavu wa kudumu baada ya kumkata mkono wa kulia na kumjeruhi katika baadhi ya viungo vyake kutokana na wivu wa kiampenzi.
Licha ya Mtuhumiwa kufikishwa mbele ya Sheria,Wanawake wilayani Humo wametakiwa kutetea haki zao huku wakiomba sheria ichukue mkondo wake dhidi ya ukatili huo uliofanywa na Bw. Ally Burian ambae anashiliwa na Jeshi la Polisi.

Mratibu wa Asasi ya kutetea wanawake na watoto(Liwopac)Bi Hidaya Chikawe alieleza kuwa licha ya harakati zinazofanywa na wanawake kuelimisha jamii Bado Vitendo hivyo vinashika kasi wilayani humo.

Hakika kwa tukio hili ni Ishara tosha inayodhihirisha kuwepo kwa ukatili wilayani humu,Hapo Awali tulizoea kusikia katika mikoa ya wenzetu lakini sasa Dunia imebadilika tunashuhudia matukio haya mara kwa mara”alieleza Chikawe.
 Aidha aliwataka akina mama wa liwale kuanza kujitetea kwa kufichua uhalifu unaojitokeza kutokana na Takwimu ya mwaka jana inaonyesha matukio hayo kuwepo kwa 2% lakini sasa hali inaongezeka kila mara hususan kipindi hiki cha mauzo ya korosho.
 Kwa Upande wao baadhi ya akinamama walisema licha ya historia ya matukio mabaya kutokea wilayani humo
wameguswa na tukio hilo huku wakitoa wito kwa jamii na serikali kuchukua hatua kali kwa wahusika wanaobanika na kukamatwa.
 Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamekuwa katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia ambapo hivi karibu Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi wa Polisi Bi Renatha Mzinga alianzisha kampeni ya kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na matukio hayo katika maadhimisho ya siku 16 za ukatili dhidi ya Mwanamke ambapo walifanikisha kutoa misaada na usafi katika kambi ya wazee na walemavu.

No comments: