MAAJABU YA
ULIMWENGU, MBWA AZAA SUNGURA NA KUMNYONYESHA
HUKO KENYA
![]() |
Mbwa akiwa na mwanasungura |
WENYEJI
wa kijiji cha Kithenge kutoka wilaya ya Igembe kusini nchini Kenya wamebaki
vinywa wazi kufuatia tukio la kustaajabisha ambapo mbwa amejifungua sungura
badala ya mbwa wa kawaida.
Kulingana
na mwenye mbwa huyo Bw Josphat Kairithia, kitendo hiki kilitokea Jumanne
wiki iliyopita ambapo alimkuta mbwa huyo akimyonyesha na akadhania ni mbwa wa
kawaida.
Baada
ya kuchunguza zaidi, aligundua kuwa hakuwa mbwa wa kawaida bali sungura na hapo
ndipo alianza kuwaita majirani waje kushuhudia tukio hilo.
Hata
hivyo, waliokuja walishtuka zaidi na wengine wakitoroka wakidhania kuwa hayo
yalikuwa mazingaombwe.
Kairithia
aliongeza kuwa mbwa huyu aliendelea kumnyonyesha sungura huyo kama kawaida na
kumpa ulinzi wa mwana.
“Tukio
hili limenishangaza sana na siwezi nikaeleza kilichotendeka. Anamnyonyesha
sungura huyu kama kawaida na hataki kumuona mtu akimkaribia. wanaokuja kumwona
lazima wapitie kwangu ili niweze kumtuliza mbwa huyo la sivyo wakiona cha mtema kuni,” akasema.
Kairithia
alitupilia mbali uwezekano kuwa hayo yangekuwa mazingaombwe huku akielezea
kuwa huenda ikawa ni ujumbe kutoka kwa mungu kuwaambia watu wapende
maadui wao.
“Siwezi
nikasema kuwa haya ni mazingaombwe kwani najua ya kwamba mungu ana njia nyingi
za kuongea na watu wake. Labda anataka kutuelezea jinsi ambavyo tunapaswa
kuwapenda hata wale ambao tunafikiri ni maadui wetu,” akasema.
Ametupilia
mbali fununu za watu ambao wanadai kuwa huenda alimwekea mbwa huyo sungura huyo
akisema kuwa hakuwa karibu mambo hayo yakitendeka.
Ili
kutoa thibitisho kwa watu, Kairithia alimwekea sungura mwingine karibu na mbwa
huyo na kilichowashangaza wengi ni kuwa hakupoteza muda kumla.
Mamia
ya watu wanazidi kutembelea familia hiyo kwa nia ya kuyaona maajabu hayo ya
ulimwengu.
No comments:
Post a Comment