UEFA CHAMPIONS LEAGUE, CHELSEA YAFUNGWA LAKINI YASONGA, ASERNAL KIDEDEA LAKINI BADO, BARCELONA CHALI LAKINI YAFUZU
Barcelona, wakicheza bila ya Nyota wao Lionel Messi na ambao kabla ya Mechi yao ya Jana walikuwa wameshatinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, walifungwa Bao 2-1 na Ajax huko Amsterdam na hicho ni kipigo cha kwa kwanza kwao Msimu huu chini ya Meneja wao mpya Gerardo Martino.
Ajax sasa watasafiri kwenda Italy Mwezi ujao kucheza na AC Milan ambao Jana waliitandika Celtic 3-0 huko Scotland na Matokeo ya Mechi hii kuamua nani ataungana na Barca.
Katika Kundi F, Timu 3, Arsenal, Napoli na Borussia Dortmund, zina uwezo wa kupata Nafasi mbili za kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 baada Arsenal kuifunga Olympique Marseille 2-0 na Borussia Dortmund kuichapa Napoli 3-1.
Arsenal watamaliza Ugenini na Napoli na Dortmund pia wako Ugenini kucheza na Marseille ambayo imeshaaga Mashindano.
Mechi za Jana za Kundi G zote zilimalizika kwa Sare ya 1-1 wakati lakini moja kati ya Zenit St Petersburg na Porto bado zina nafasi ya kuungana na Atletico Madrid Raundi ijayo.
MATOKEO:
Jumanne
26 Novemba 2013
FC
Steaua Bucureşti 0 FC Schalke 0
FC
Basel 1 Chelsea 0
Arsenal
2 Olympique de Marseille 0
Borussia
Dortmund 3 SSC Napoli 1
FC
Porto 1 FK Austria Wien 1
Football
Club Zenit 1 Club Atlético de Madrid 1
Celtic
FC 0 AC Milan 3
AFC
Ajax 2 FC Barcelona 1
TIMU
ZILIZOFUZU KUINGIA Raundi ya Mtoano ya Timu 16:
[Timu
5 Bado 11]
-Bayern
Munich
-Manchester
City
-Atletico
Madrid
-Barcelona
-Chelsea
RATIBA
YA LEO
Jumatano
27 Novemba 2013
Bayer
04 Leverkusen v Manchester United FC
FC
Shakhtar Donetsk v Real Sociedad de Fútbol
Real
Madrid CF v Galatasaray A.Ş.
Juventus
v FC København
RSC
Anderlecht v SL Benfica
Paris
Saint-Germain v Olympiacos FC
PFC
CSKA Moskva v FC Bayern München [20:00]
Manchester
City FC v FC Viktoria Plzeň
No comments:
Post a Comment