ALIYEBAKA PUNDA AFUNGWA JELA MIAKA HUKO NCHINI KENYA
![]() |
| James Mwangi |
MAHAKAMA
ya Nyeri nchini Kenya jana imemhukumu mwanaume aliyepatikana na hatia ya
kushiriki kitendo cha ngono na punda miaka sita jela.
James
Mwangi alipatikana na hatia ya kutenda kosa hilo Aprili 26 katika kijiji cha Ruring’u
maeneo ya Nyeri na kulingana na Hakimu mkuu wa Nyeri Bi Wilbroda Juma,
mashahidi walitoa ushahidi wa kutosha kudhihirisha kuwa Mwangi alishiriki
kitendo hicho
Bi
Juma alisema kuwa mwenye punda Bw Peter Mathenge, alikuwa mmoja wa mashahidi na
alieleza mahakama hiyo kuwa alimwacha punda huyo na punda wengine wachanga
malishoni lakini akafahamishwa baadaye na jirani kuwa Mwangi alipatikana
akifanya kitendo hicho kwa punda huyo.
Bw
Mathenge alisema kwamba alielekea katika eneo alimokuwa ameelekezwa na jirani
yake na kupata mipira ya kondomu katika eneo ambalo punda wake alitendewa uovu
huo. Hapo ndipo aliamua kuwafahamisha maafisa wa polisi.
Maafisa
wa polisi pia walitoa ushahidi katika mahakama hiyo na kuelezea kuwa walimhoji
mmoja wa walioshuhudia tukio hilo aliyejitambulisha kama Bw Ng’ang’a na akasema
kwamba aliona punda huyo akiwa amefungwa miguu na Mwangi huku akitekeleza
kitendo hicho cha ngono kwa punda huyo.
Maafisa
hao wa polisi walipata mpira wa kondomu katika sehemu nyeti za punda huyo
walipokuwa wanafanya uchunguzi kuhusu kesi hiyo.
Akijitetea
mbele ya mahakama hiyo, Mwangi alieleza kuwa yeye ni kijana shupavu mwenye
bidii na akaomba apewe kifungo cha miaka michache kwani ana uwezo wa kutegemewa
siku zijazo kwa kuleta maendeleo katika jamii.
Mwangi
alieleza kuwa hajawahi kushiriki kwa kutenda ouvu madai ambayo yalithibitishwa
na mwendesha mashtaka Bi Cathrine Murugi aliyesema kwamba Mwangi hana historia
ya kutotii sheria kwa kutenda maovu.
Hakimu
Bi Juma alieleza kuwa amesikia tetesi zake Mwangi lakini Mahakama ilikuwa
imempata na hatia ya kuhukumiwa.
Bi
Juma alisema kwamba ni jambo la kushangaza kuwa visa vya watu kutenda maovu
kama hayo kwa wanyama vinaendelea kuongezeka katika eneo hilo.
Hakimu
huyo alisema kuwa wanaopatikana na hatia kama hiyo wanafaa kuadhibiwa vikali
ili wawe funzo kwa wengine katika jamii.
“Umepatikana
na hatia na kuhukumiwa miaka sita jela,”akasema Bi Juma.

No comments:
Post a Comment