TANZANIA YAZIDI KUPOROMOKA VIWANGO VYA FIFA
SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetoa orodha mpya ya
viwango vya ubora kwa mwezi huu huku Tanzania ikizidi kudidimia kwa kuporomoka
kwa nafasi mbili.
Katika orodha hizo Tanzania imeshuka mpaka katika
nafasi ya 129 kutoka nafasi ya 127 waliyokuwepo mwezi uliopita. Kwa upande wa
Afrika Ivory Coast wameendelea kuongoza kwa kushika nafasi ya 17 katika orodha
hizo duniani wakifuatiwa na Ghana ambao wanashika nafasi ya 23 huku Algeria nao
wakiwa katika nafasi ya 32. Mabingwa wa Afrika Nigeria wanashika nafasi ya
nne kwa kushika nafasi ya 33 na tano bora kwa upande wa Afrika inafungwa na
Mali walioko katika nafasi ya 41. Mabingwa wa dunia Hispania wameendelea
kubaki katika nafasi ya kwanza kwenye orodha hizo wakifuatiwa na Ujerumani
waliopanda mpaka nafasi ya pili na kuiondoa Argentina iliyopo katika nafasi ya
tatu. Nafasi ya nne katika orodha hizo inashikiliwa na Colombia ambao
wamepanda kwa nafasi moja kulinganisha na walipokuwa mwezi uliopita huku
Ubelgiji wakifunga tano ya orodha hizo.
SABA BORA KATIKA ORODHA ZA FIFA KUONGOZA DROO ZA UPANGAJI RATIBA YA KOMBE LA DUNIA BRAZIL.
SWITZERLAND itakuwa mojawapo ya nchi nane
zitakazoongoza droo ya ratiba ya michuano ya Kombe la Dunia 2014 itakayofanyika
Desemba mwaka huu baada ya kukwea mpaka nafasi ya saba katika orodha za ubora
dunia zilizotangazwa leo. Hispania, Argentina, Ujerumani, Colombia,
Ubelgiji na wenyeji Brazil nao pia wataongoza droo hiyo wakiungana na Uruguay
kama wakifanikiwa kuwafunga Jordan katika mechi za mikondo miwili za mtoano
mwezi ujao. Kama Uruguay ikishindwa kufuzu michuano hiyo, Uholanzi ambao
wanashika nafasi ya nane katika orodha hizo sambamba na Italia itachukua nafasi
hiyo. Katika kanuni za Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Brazil ukijumlisha
na timu saba zilizopo katika orodha za juu za shirikisho hilo ndio zitaongoza
droo ya upangaji ratiba ya michuano hiyo.
No comments:
Post a Comment