MWANAMKE ASHITAKIWA KWA KUMNYONYESHA MTOTO WA JIRANI HUKU AKIWA NA VIRUSI VYA HIV
MWANAMKE raia wa Zimbabwe aliyenyonyesha mtoto wa jirani bila ruhusa anakabiliwa na kifungo cha karibu miaka miwili kwa kumwambukiza mtu virusi vya HIV kimakusudi baada ya kupatikana na virusi hivyo.
Annie
Mpariwa, 39, alifikishwa mbele ya mahakama ya Gaborone mnamo Jumatano na kesi
hiyo kuahirishwa hadi Oktoba 24 kuruhusu kipimo cha pili cha HIV kufanyiwa
mtoto huyo.
Matokeo
ya kwanza ya mtoto huyo yalionyesha hana virusi ilhali mama huyo yalikuwa na
virusi.
Mpariwa
alikamatwa wiki jana kwa mashtaka ya usumbufu na iwapo mtoto huyo atapatikana
na virusi mashtaka hayo yatazidishwa hadi 'kumwambukiza mtu mwingine HIV
kimakusudi.
Mama
ya mtoto huyo wa miezi 14, Nyasha Mironga, alisema kumwona mwanawe
akinyonyeshwa na jirani wake ni jambo lilimshtua sana.
Kisa
hicho kimetokea baada ya kupitishwa kwa sheria mpya ya HIV/Aids inayotoa adhabu
kali zaidi kwa wale wanaowaambukiza wengine HIV kimakusudi.
Africa review.
No comments:
Post a Comment