MWANAMKE MBABE
ALIYEJARIBU KUMPA SUMU MUMEWE ILI AFE, AENDA JELA MIAKA MITATU.
![]() |
Bw Charles Mbaruku Kimani |
MWANAMKE
mmoja amefungwa jela miaka mitatu na mahakama ya Murang’a kwa kujaribu kumpa
sumu mumewe na kumpiga.
Bi
Purity Wanjiku Mbaruku, 30, ambaye ni mama wa watoto wanne alishtakiwa kwa
makosa mawili mbele ya Hakimu Mkuu mkazi Bw Joseph Masiga.
Katika
shtaka la kwanza, Bi Wanjiku alishtakiwa kuwa mnamo Agosti 24 mwaka huu katika
kijiji cha Matongu, lokesheni ya Kimathi eneo la Kiharu, alijaribu kumpa sumu
mumewe Bw Charles Mbaruku Kimani.Vile vile alishtakiwa kwa kumpiga na kumjeruhi
mumewe.
Katika
shtaka la kwanza, kiongozi wa mashtaka Bw Paul Gathara alieleza mahakama kuwa mshtakiwa
alimkaba koo mumewe na kujaribu kumnywesha dawa ya kuua kupe aina ya ‘Tria-Tix’
saa nne na nusu usiku.
Alielezea
mahakama kuwa Bi Wanjiku alikusudia kumwua Bw Kimani kwa kumpa sumu hiyo
hatari.
“Hata
hivyo mlalamishi alimuuma mshtakiwa mkono na akapiga yowe na majirani wakaja,” alisema Bw Gathara
Ijumaa.
Mahakama
ilielezwa kwamba Bw Kimani,54, alitoa ripoti katika kituo cha polisi cha Kabuta
mara moja na kutumwa katika kituo kikuu cha polisi Murang’a mjini na kisha
baadaye kwenda hospitali kuu ya Murang’a ambapo alitibiwa.
Baada
ya kuandikisha ripoti, alipewa fomu ya polisi ya P3 kuonyesha kwamba alipata
majeraha na polisi wakamkamata mkewe hapo siku ya Alhamisi.
Akijitetea,
mwanamke huyo wa umri wa miaka 30 alisema walikuwa wakizozana kwa miaka mingi
tangu aolewe na Bw Kimani miaka 13 iliyopita na amepata ugonjwa wa shinikizo la
damu kufuatia ugomvi wa kila saa.
“Yeye
ndiye aliyetaka kunipa sumu na amefanya tuzozane kwa miaka mingi mpaka nikapata
ugonjwa wa shindikizo la damu,” aliambia mahakama.
Lakini
hakimu Masiga alisema kosa hilo ni kubwa mno kwani lingepelekea kifo cha
mlalamishi akiongeza mshtakiwa alifaa kupata adhabu kali.
Alimfunga
miaka miwili kwa kosa la kwanza na mwaka mmoja kwa shtaka la pili.
Bw
Kimani alifurahia uamuzi wa mahakama na kusema ataenda katika afisi
inayosimamia maswala ya watoto na kudai wanawe wawili aliozaa na mkewe ambao
wanaishi na nyanya yao huko Kaunti ya Kirinyaga.
Vile
Vile aliandikisha ripoti katika kituo cha polisi cha Murang’a akidai amepokea
vitisho kutoka kwa shemeji yake mmoja kwa njia ya simu.
“Nilipigiwa
simu na ndugu mmoja wa bibi yangu ambaye anaishi Kimicha kaunti ya Kirinyaga na
akanionya kuwa nitakiona cha mtema kuni kwa kumshtaki dadake,” aliambia polisi
mnamo Alhami.
Swahili hub
No comments:
Post a Comment