MFALME MSWATI KUOA MKE WA 14
Msemaji
wa ikulu ya Swaziland amesema Mfalme Mswati
III amemteua mwanamke wa umri wa miaka 18 anayeshindania tuzo ya urembo kumuoa
awe mke wa 14
"Ninaweza
kuthibitisha kwamba mfalme ameletea taifa liphovela mpya (liphovela ni
mchumba wa kifalme),” gavana wa ikulu ya Ludzidzini Timothy Mtetwa alisema.
Mswati,
mwenye umri wa miaka 45 ndiye mfalme wa pekee aliyesalia mwenye mamlaka makuu
Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
Kwa
mujibu wa Mtetwa, Mfalme Mswati III alimtambulisha mwanamke huyo kwa jina
Sindiswa Dlamini wakati wa Densi ya Tete.
Alikuwa
amevalia manyoya mekundi kichwani – ishara ya ufalme.
Mwanamke
huyo alimaliza shule ya upili ya St. Francis High School mjini Mbabane mwaka uliopita
na akafika fainali ya shindano la urembo la Miss Cultural Heritage. Mshindi
atatangazwa Septemba 28.
Harusi
itafanyika tu ikiwa mchumba huyo atashika mimba. Dlamini wakati huo atakuwa mke
wa 14 wa Mswati.
Wake
watatu wametoroka nyumba ya mfalme huyo miaka ya hivi karibuni.
Wa
majuzi zaidi, Malkia LaGija, alitoroka ikulu 2012 akidai kwamba alikuwa
akichapwa na kuteswa kiakili.
Mwingine,
LaDube, anadaiwa kupigwa baada ya kupatikana akishiriki ngono na waziri wa
haki, ambaye ni rafiki wa karibu wa mfalme huyo.
Mswati
alimteka nyara na kumuoa mfalme huyo akiwa na umri wa miaka 16 mwaka 2005.
No comments:
Post a Comment