MWANAUME ADAI MKEWE ALITAKA KUMNYWESHA SUMU ILI AFE HUKO NCHINI KENYA
![]() |
| Bw Charles Mbaruku Kimani |
Swala la unyanyasaji dhidi ya wanaume nchini Kenya unaendelea kushika kasi baada ya mwanamume
mmoja kunusurika kifo baada ya mkewe kumlazimisha kunywa sumu.
Bw
Charles Mbaruku Kimani kutoka kijiji cha Matongu kata ya Kimathi eneo la Kiharu
alidai mkewe alimpiga dafrau usiku na kutaka kumnywesha sumu kwa nguvu lakini
akakataa.
Akiongea
katika kituo cha polisi mjini Murang’a
ambapo aliandikisha ripoti, jamaa huyo wa miaka 54 alidai mkewe ana mazoea ya
kumshambulia akishirikiana na mwanawe wa kiume.
Bw
Kimani alisema wameoana kwa miaka 13 na wamekuwa wakizozana kwa siku nyingi
huku mkewe akitoroka kwa wazazi wake mara kadhaa katika kijiji cha Kimicha.
Alisema
kuwa siku ya Jumamosi usiku, mkewe alichanganya dawa ya kuua kupe na kuitia kwenye
chupa na kumkaba koo mzee huyo huku akitaka anywe dawa hiyo ili afe.
“Tulikuwa
tumetoka safari na ndani ya nyumba kulikuwa na giza kwani hatukuwa tumewasha
taa na nilikuwa nimeketi kitini wakati mke wangu aliponishambulia,”
alisema Bw Kimani ambaye alitibiwa hospitali kuu ya Murang’a baada ya kisa
hicho.
Mwanamme
huyo ambaye anafanya biashara ya kuuza changarawe alidai mkewe alimshika kwenye
sehemu ya shingo na kuelekeza chupa hiyo iliyojaa sumu kwenye mdomo wake lakini
mwanamme huyo akamuuma mkewe mkono wakati wa kisa hicho.
Hata
hivyo, kiasi kidogo cha sumu kiliingia mdomoni na akalazimika kukimbizwa
hospitali ili kuzuia maafa zaidi.
Sehemu
ya mdomo ilionekana ikiwa imechomwa na dawa hiyo huku akiongezea alianza kuumwa
na tumbo baada ya kutiwa sumu hiyo mdomoni.
“Nilipomuuma
mke wangu mkono,alipiga mayowe na majirani wakafika na kunipa maji nikabugia
mdomoni ili nisife,” alisema Bw Kimani.
Alisema
ameandikisha ripoti katika kituo cha polisi cha Murang’a huku akiongeza mkewe
alitorokea kwao nyumbani Kirinyaga na baadhi ya mali yake.
Mwanamme
huyo alisema alimwoa mkewe akiwa na watoto wawili na hapo baadaye wakazaa
wengine wawili.
Hata
hivyo alisema mkewe na mwanawe mmoja wa kiume wamekuwa na mazoea ya
kumashambulia na kusambaratisha biashara yake ya duka
Aliongezea
kuwa anahofia usalama wake kwani anashuku mkewe anaweza panga njama ya kumuua.
Swahili hub

No comments:
Post a Comment