MAN UNITED NA CHELSEA HAKUNA MBABE
![]() |
Cole akikabiliana na Rooney |
![]() |
Mourihno na Moyes wakipongezana |
Mchezo wa
ligi kuu nchini uingereza kati ya miamba wawili Man United na Chelsea usiku wa
kuamkia leo umemalizika kwa sare ya bila kufungana kwenye Uwanja wa Old
Trafford.
Rooney
alianza katika kikosi cha kwanza baada ya tetesi za muda mrefu majira haya ya
joto kwamba atajiunga na Jose Mourinho Magharibi mwa London, lakini alipiga
soka ya uhakika akiwa na uzi mwekundu.
Chelsea
ilianza bila washambuliaji wake Fernando Torres na Romelu Lukaku walioanzia
benchi, lakini gumzo zaidi ni kila upande kulalamikia kunyimwa penalti katika
mechi hiyo.
Katika mchezo huo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Enlgand baina ya timu hizo, United ilianzisha washambuliaji watatu, Welebeck, Rooney na Van Persie.
Katika mchezo huo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Enlgand baina ya timu hizo, United ilianzisha washambuliaji watatu, Welebeck, Rooney na Van Persie.
Dakika ya
65 Lampard alishika kabisa mpira kwenye eneo la hatari kufuatia shuti la
Cleverley, lakini refa 'akapeta'.
Dakika ya
71 Ashely Cole alianguka kwenye eneo la hatari wakati akikabiliana na Jones na
akalilia penalti na hata Mournho akaonekana kulalamika akiwa kwenye
benchi.
Mchezo ulikuwa
mkali na timu hizo zilishambuliana kwa zamu na baada ya mechi wachezaji
walipongezana kwa mchezo mzuri.
Jose
Mourinho alisema baada ya mechi mchezo ulikuwa wa haki na hadhani kama kuna
iliyomzidi mwenzake uwezo, wakati Moyes alilalamikia penalti ya Lampard kuunawa
mpira na kuwapongeza vijana wake kwa soka nzuri.
No comments:
Post a Comment