Tuesday, July 30, 2013

TIMU YA AL MASRY YAONDOLEWA ADHABU YA KUFUNGIWA KUTONA NA VURUGU ZA PORT SAIED
CHAMA cha Soka nchini Misri-EFA kimetangaza kuiondolea adhabu timu ya Al Masry kwa kuiruhusu kushiriki msimu mpya wa Ligi Kuu nchini humo ambayo inatarajiwa kuanza Agosti 22 mwaka huu. 
Al Masry walifungiwa mwaka mmoja na EFA baada ya vurugu zilizotokea Port Saied Februari mwaka jana ambapo mashabiki zaidi ya 72 wa Al Ahly waliuawa uwanjani. 
Msemaji wa EFA Azmy Megahed amesema Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo ya CAS imeiruhusu Al Masry kucheza na tayari wameshalipa ada yao ya ushiriki katika ligi hiyo. 
Hata hivyo Al Masry watakabiliwa na tatizo la kutafuta uwanja mwingine wa kutumia katika mechi zao za nyumbani kutokana na adhabu ya kufungiwa miaka mitatu uwanja wao wa Port Saied ikiwa bado haijamalizika. Maofisa awa Al Masry wanataka mechi zao kuchezwa Al Ismailiya lakini majeshi ya ulinzi walikataa wazo hilo kwasababu za kiusalama.

CAF YATUPILIA MBALI OMBI LA AL AHLY KUSOGEZA MECHI YAO DHIDI YA ORLANDO PIRATES.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limetupilia mbali maombi ya Al Ahly waliotaka kusogeza mbele mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa ya Afrika dhidi ya Orlando Pirates iliyotakiwa kuchezwa Agosti 4 kwa ajili ya mfungo wa Ramadhan.
Katika taarifa ya klabu hiyo iliyotumwa katika mtandao wake walithibitisha kupokea barua kutoka CAF ya kukataliwa ombi lao hilo. Mapema Jumapili iliyopita mkurugenzi wa michezo wa Al Ahly Sayed Abdel Hafiz aliviambia vyombo vya habari nchini Misri kuwa klabu hiyo imeomba mchezo huo kusogezwa mbele kwa siku tano ili kuepuka matatizo wachezaji wake waliyokutana nayo katika mchezo dhidi ya Zamalek. Hafiz alidai kuwa wachezaji wake walikabiliwa na wakati mgumu katika mchezo huo baada ya kukataa kufungua na kucheza mchezo huo katika kipindi cha mchana kilichokuwa na joto kali. 
Klabu hiyo pia imetakiwa kutafuta uwanja mwingine kwa ajili ya mchezo huo wa kundi A baada ya jeshi kuwakatalia uwanja wao wa Air Defence uliopo jijini Cairo kwasababu za kiusalama

No comments: