Tuesday, June 18, 2013

MWANAMUME AKAMATWA KWA KUSHIRIKI NGONO NA NG'OMBE
Mfanyakazi wa Kampuni ya Kusambaza Maji Kikuyu, aliyetambuliwa kwa jina Kariuki baada ya kutiwa mbaroni Juni 12, 2013
MAHAKAMA ya Kikuyu nchini Kenya  ilimwachilia huru mwanaume aliyesemekana kuwa alishiriki kitendo cha ngono na ng’ombe kwa dhamana ya Sh10, 000 huku wakingojea uchunguzi zaidi dhidi ya shtaka hilo.
Bw Justin Kariuki aliachiliwa na polisi wa Kikuyu ambao wanaendeleza uchunguzi kuhusu madai ya wanavijiji wa Mugumo-ini waliosema kuwa mzee huyo alikuwa amezoea tabia ya kushika ng’ombe.
Inadaiwa kufumaniwa akichafua ng’ombe wa tatu.
Polisi wanashuku mzee huyo anasingiziwa kwani wakazi wengi wa Mugumo-ini huiba maji ya kampuni ya Kikuyu Water na wengine wako na deni kubwa katika kampuni hiyo ambayo Bw Kariuki anafanyia kazi.
Mpema wiki hii mwanaume huyo  alikamatwa na polisi Kikuyu, Kiambu baada ya kudaiwa kushiriki ngono na ng’ombe mwenye mimba eneo la Kiambaa.
Mwenye ng’ombe bwana David Munene aliomba mzee huyo atozwe faini ya Sh150, 000 akisema hawezi tena kuendelea kumfuga ng’ombe huyo au kunywa maziwa yake.
Munene alisema kuwa ngombe huyo ana mimba ya miezi saba na alishtuka sana kupata mzee huyo akifunga suruali yake ndefu huku akiwa na kinyesi cha ng’ombe nguoni mwake baada ya kufanya ngono na mnyama huyo.
Aliongeza kuwa mshukiwa alikuwa amechukua viti viwili ambavyo wao hukalia wakati wanakamua ngombe, na kuviwekelea kimoja juu ya kingine ili afikie ngombe vizuri na kufanya kitendo hicho cha aibu.
“Nilimpata tu akifunga suruali yake ndefu na akajaribu kutoroka lakini tulimshika na kujulisha polisi,” alisema Bw Munene.
Ilisemekana kuwa Kariuki ameajiriwa katika Kampuni ya Maji ya Kikuyu na hutembea nyumbani mwa watu akiangalia kiasi cha maji ambacho watu wametumia kazi ambayo hujulikana kama kusoma mita.
Bi Mary Nyambura alisema kuwa kama familia wanataka mzee huyo alipe Sh100, 000 kwa ngombe huyo, na Sh50 ,000 kwa ajili ya ndama aliye tumboni kisha mshukiwa achukue ngombe huyo kuwa wake.
Mkuu wa Polisi Joshua Opiyo alithibitisha tukio hilo na kusema alitiwa nguvuni  katika stesheni ya polisi ya Kikuyu, lakini bado ngombe yumo kwenye zizi la mwenyewe,” alisema Bw Opiyo.
Alikubaliana na familia kuwa ni jambo la kuchafua roho kunywa maziwa ya ngombe yule, lakini akaomba wenye ngombe kusubiri uamuzi wa korti.
Ilibidi polisi kutumia vitoa machozi kuwatawanya watu ambao walikuwa wamejaa mahali ambako tukio hilo lilifanyika katika kijiji cha Migumo-ini wakitaka kumpiga mzee huyo.
Mkaazi wa Mugumo-ini, Paul Munga alisema ni mara ya tatu mzee huyo kumdhulumu ng’ombe.
“Alikuwa ameshika ng’ombe wa mamangu lakini hakupata kifungo, aliachiliwa na kuendelea na tabia yake,” alisema Bw Munga.
Wakazi wana hofu kuwa Kariuki ataachiliwa tena, lakini wamesema, “Kariuki asifike kijiji cha Migumo-ini tena kwani anatuharibia ngombe zetu.”
Wakazi wengine hata walisema atolewe sehemu zake za siri kama funzo kwa wengine na kukomesha tabia zake mbaya

swahilihub.com

No comments: