FAINALI YA WAJERUMANI WATUPU WEMBLEY
LIGI YA MABINGWA BAADA YA BAYERN KUIKUNG'UTA 3-0 BARCA CAMP NOU NA KUFUZU KWA
JUMLA YA 7-0
![]() |
Bao la kwanza la Robben |
![]() |
Arjen Robben (katikati) akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza |
![]() |
Sasa ndo umefanya nini, Kipa wa Barca, Victor Valdes akilalamika baada ya Pique kujifunga |
Itakuwa fainali ya
Wajerumani watupu Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Wembley wiki tatu zijazo
Jumamosi, ikiwakutanisha Bayern Munich na Borussia Dortmund.
Hiyo inafuatia
Barcelona kutandikwa mabao 3-0 nyumbani usiku wa leo, baada ya awali kuchapwa
4-0 Ujerumani, hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 7-0.
Barcelona
walionekana kabisa kuzidiwa uwezo na mapema tu walionekana hawawezi kupanda
mlima huo. Mabao ya Bayern ambao tayari ni mabingwa wa Ujerumani, wakiivua taji
Dortmund, yamefungwa na Arjen Robben dakika ya 49, Gerard Pique
aliyejifunga dakika ya 72 na Thomas Muller dakika ya 7.
No comments:
Post a Comment