AMA KWELI NDOA NDOANO,
MKE AMSHUSHIA KIPIGO MUMEWE BAR BAADA YA
KUTOONEKANA NYUMBANI
Mume na mke wakionyeshana ubavu |
Mwanamke mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, hivi
karibuni alizua sekeseke la aina yake baada ya kumvaa mwanaume anayedaiwa ni
mume wake na kumshushia kichapo.
Tukio hilo la aina yake lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Baa ya Corner iliyopo Afrikasana, Sinza jijini Dar ambapo inadaiwa chanzo cha vurumai hilo ni mwanaume huyo kutoonekana nyumbani.
Tukio hilo la aina yake lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Baa ya Corner iliyopo Afrikasana, Sinza jijini Dar ambapo inadaiwa chanzo cha vurumai hilo ni mwanaume huyo kutoonekana nyumbani.
Habari kutoka eneo la tukio hilo
zinasema kuwa, awali mwanamke huyo
alifika katika katika eneo hilo asubuhi na mapema huku akionekana
kuangazaangaza huku na kule kabla ya kukutana na bwana wake huyo na kuanza
kuzozana.
“Yule mwanamke alipofika hapa alionekana alikuja kishari na hata alivyokuwa akiongea na yule bwana wake tulibashiri kutokea kwa ugomvi.
“Yule mwanamke alipofika hapa alionekana alikuja kishari na hata alivyokuwa akiongea na yule bwana wake tulibashiri kutokea kwa ugomvi.
“Kweli haukupita muda mrefu tukaona
wakianza kukunjana, mara mwanamke akapandwa na hasira na ndipo sekeseke la aina
yake likatokea,” kilidai chanzo hicho.
Ikaelezwa kuwa kutokana na jinsi walivyokuwa wakitifuana, wasamaria wema
waliingilia kati na kuwataka wayamalize badala ya kuwapa faida watu.
Kufuatia ushauri huo, wawili hao waliachiana na mwanamke akaanza kulia kisha akamlalia mwanaume huyo kifuani, wakabembelezana na kuondoka eneo hilo.
Kufuatia ushauri huo, wawili hao waliachiana na mwanamke akaanza kulia kisha akamlalia mwanaume huyo kifuani, wakabembelezana na kuondoka eneo hilo.
Global publisher.
No comments:
Post a Comment