Wednesday, April 17, 2013

  BI KIDUDE HATUNAYE TENA DUNIANI
Bi - Kidude
Mwanamuziki mkongwe wa Muziki wa Mwambao nchini na barani Afrika Fatuma Binti Baraka maarufu kwa jina la Bi Kidude amefariki mchana huu akiwa na umri zaidi ya miaka 90.

Taarifa zinadai kuwa Bi Kidude amefariki majira ya saa 7 mchana wa leo nyumbani kwa ndugu yake huku Bububu Kisiwani Zanzibar.

Aidha taarifa hizo zinaelezo kuwa Mipango yua kuusafirisha mwili wa Marehemu inafanyika kutoka huko Bububu hadi Nyumbani kwake Raha Leo.

Bi Kidude alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa na kulazwa mara kadhaa lakini kifo chake kinaelezwa pia kuchangiwa zaidi na umri mkubwa.

Msiba huu ni mzito kuwahi kutokea kwa tasnia ya muziki na Sanaa kwa ujumla kufuatia Mchango mkubwa wa Marehemu katika kukuza muziki halisia wa mwambao.

Rais Jakaya Kikwete alimtunuku Bi Kidude Nishani ya Uhuru wa Tanzania kwa mchango wake mkubwa alioutoa katika kipindi cha uhai wake.
Nasi tunaungana na watanzania wote na wapenzi wa burudani ulimwenguni kwa msiba huu mzito.

Bi Kidude alizaliwa maeneo ya Mferejimaringo Zanzibar. Alianza muziki mwaka 1920 akiwa na miaka 13. Ni miongoni mwa wasanii wakongwe hapa nchini wenye historia ya kipekee. Licha ya kuwa na historia ya kipekee, msanii huyo mkongwe amejipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi kupitia kazi yake ya sanaa.

Bikidude anaminika kwamba ndie msanii mkongwe kuliko msanii mwingine yoyote wa kike hapa nchini.

Msanii huyo ni muimbaji mwenye historia ya kipekee hapa nchini na kutokana na umahiri wake wa uimbaji na amefanikiwa kutembea nchi mbalimbali za Afrika, Ulaya na Asia kwa ajili ya kufanya kazi zake za muziki na kuitangaza taifa kwenye jumuia za kimataifa.

Katika siku za hivi karibuni, mkongwe huyo alikuwa akisumbuliwa na maradhi lakini kwa sasa hali yake inaendelea vizuri ingawa hajaanza kufanya shughuli zake za muziki.

Msanii huyo mwishoni mwa mwaka jana, serikali ilimtunukia nishani ya heshima kutokana na mchango wake mkubwa kwa taifa. Nishani hiyo alitunukiwa na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu mjini Dar es Salaam.

Rais Kikwete alimtunuku Bikidude na wasanii wengine nishani ya sanaa na michezo ambayo hutolewa kwa wasanii na wanamichezo mashuhuri, ambao kazi zao za sanaa au michezo zimeipatia sifa kubwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Anaangaliwa kama malkia wa muziki wa taarab na unyago hapa nchini ambaye kipaji chake kiligunduliwa na kuimarishwa na mkongwe wa muziki wa aina hiyo Siti binti Saad kati ya miaka ya 1880 mpaka 1950.

Mpaka sasa haijafahamika tarehe ya kuzaliwa ya bibi huyo kwasababu sehemu kubwa ya historia zinazo husu historia ya maisha yake hazioani na hivyo kuwepo na taarifa ambazo ni za kubuni.

Mwaka 2005, Bikidude alipewa tuzo ya heshima ya dunia WOMEX tuzo ambazo zilibuniwa mwaka 1999 na mbazo wanazawadiwa watu ambao wamepata mafanikio makubwa katika muziki au wametoa mchango mkubwa katika muziki, umuhimu wa mtu katika jamii na hata, mafanikio ya kibiashara na kwa upande wake ilitokana na mchango wake katika muziki na utamaduni wa Zanzibar.

Akiwa mdogo, Bikidude alisifiwa sana kutokana na sauti yake na katika miaka ya 1920 alianza kuimba na vikundi mbalimbali vya kiutamaduni.

Alipokuwa na umri wa miaka 13, baada ya kulazimishwa kuolewa aliamua kutoroaka na kuelekea Tanzania Bara.
Bikidude ni moja ya waimbaji wakongwe waliozunguka nchi zote za Afrika Mashariki akiimba taarab ambapo alitembelea miji mikubwa ya ukanda wa pwani pamoja na bara upande wa ziwa Victoria na Tanganyika.

Mwaka 1930, alirejea Dar es Salaam na kujiunga na kikundi cha Egyptian Taarab ambacho alidumu nacho kwa miaka mingi.
Katika miaka ya 1940 alirejea Zanzibar na kujenga nyumba yake iliyokuwa ya matope na kuanza maisha mapya hapo.

Alikuwa maarufu sana kwa shughuli za unyago ambazo ziliwaandaa masichana wadogo kuelekea katika ubalehe na kuingia katika maisha ya utu uzima.
Ni mtaalamu wa mambo hayo ya mila kongwe akifanya hivyo kwa wasichana akitumia mafunzo ya kitamaduni kuwaelekeza wasichana namna ya kuishi na waume zao na kuepuka migongano ya kifamilia na unyanyasaji wa mapenzi.

Sifa na jina la Bikidude lilikuwa na kusifika katika jamii yote ya Zanzibari na kuwa kielelezo cha utalii wa visiwa hivyo vya karafuu ambapo hoteli mbalimbali kubwa na zenye hadhi ya juu visiwani humo zimekuwa zikizipa majina migahawa ya hoteli jina la Bikidude, mfano 236 Hurumzi inatumia jina la mgahawa wake jina la 'Kidude'.

Moja ya nyimbo zake ambazo zilitamba na kumpatia umaarufu mkubwa mkongwe huyo ni Muhogo wa Jang'ombe ambao ulikamata kwenye mwambao wa Afrika Mashariki.
Bikidude ni hazina kubwa na mwalimu mzuri kwani inasemekana wasanii wengi wamepata mafunzo kutoka kwake.
Pamoja na umahiri wa msanii huyo lakini hajawahi kukumbwa na kashfa yoyote hadi sasa hivyo amekuwa na historia ya kipekee tofauti na wasanii wa sasa.

Bikidude, amedumu kwenye fani ya uimbaji kwa zaidi ya nusu karne na kwa sasa ni msanii pekee wa taarab mwenye sifa zilizotukuka kutokana na ukongwe wake na umahiri wake katika kuimba taarab.

No comments: