Tuesday, March 12, 2013


MKE AMUUWA MUMEWE KWA KISU KWA WIVU WA MAPENZI.
Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz
MWANAMKE mmoja aliyefahamika kwa jina la Happyness Mrema (28) amemchoma kisu mumewe Audiphas Mrema (30) na kumuuwa kutokana na ugomvi wa wivu wa mapenzi. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz, alisema tukio hilo lilitokea Machi 9, 2013 katika Kijiji cha Kikelelwa wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro, ambapo mwanamke huyo alimchoma kisu mumewe na kumsababishia mauti papohapo.
Kwa mujibu wa Kamanda Boaz, siku ya tukio marehemu alifika nyumbani saa moja usiku na kumkuta mkewe amenuna ndipo ulipozuka ugomvi. “Inadaiwa kuwa baada ya mume huyo kuja saa moja mke alimuhoji kwa nini amechelewa kurudi ndipo ugomvi ulipoanza ambao unaelezewa ni wivu wa
kimapenzi na hatimaye mke kumchoma kisu mumewe na kufa papohapo,” alisema.
Aidha kamanda alisema mwanamke huyo anashikiliwa na polisi na kwamba atafikishwa mahakamani wakati wowote uchunguzi utakapokamilika.

No comments: