Wednesday, March 13, 2013

BARCELONA YATINGA ROBO FAINALI KWA KISHINDO YAIBUGIZA AC MILANI 4-0
Messi
Timu ya Barcelona imetinga hatua ya robo fainali baada ya kuichakaza AC Milan mabao 4-0 na kuitoa nje ya ligi ya mabingwa mchezo ulipigwa katika dimba la Camp Nou usiku wa kuamkia leo.

Ikiwa na deni la bao mbili iliweza kusawazisha magoli yote na kufunga mengine mawili na kutoka na ushindi wa mabao manne kwa sifuri
Goli la kwanza lilipatikana  katika dakika ya tano ya mchezo na  Lionel Messi kwa shuti kali na nje ya kumi na nane.
Alikuwa Messi tena pale aliposhindilia goli la pili Dk ya 40 na  kuisaidia timu yake kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0.

David Villa alifunga bao la tatu dk ya 55 baada ya kutengenezewa pasi maridadi  na   Xavi lakini badae  Jordi Alba alihitihimisha ushindi katika dk ya 90 kwa Barca na kutoka na ushindi huo wa mabao 4-0  .
Katika mchezo mwingine timu ya Galatasaray nayo imeweza kufuzu hatua ya robo fainali baada ya kuitoa nje ya mashindano timu ya Shalke 04 mabao 3-2.
Mabao ya Gatasaray yakipachikwa na Altintop 37, Yilmaz 42, Bulut 90+4
Huku mabao ya shalk yakifungwa na Neustadter 17, Michel Bastos 63.
Mbali na Barcelona na Galatasaray Timu nyingine ambazo zimeshingia robo fainali mpaka sasa ni  Borussia Dortmund, Juventus, Paris St Germain na Real Madrid.
Michuano hiyo inaendelea tena leo kwa mechi kati ya
Bayern Munich dhidi ya Arsenal, huku Malaga wakiwakaribisha Porto.

No comments: