Monday, May 26, 2014

AFIKISHWA MAHAKAMNI KWA KUIBA PETE YA UCHUMBA YA RAFIKI YAKE NA KUMVALISHA MPENZI WAKE.

Kijana mmoja kutoka  eneo la Korogocho  Nairobi nchini Kenya amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuiba pete ya ndoa ya rafiki yake na kumvesha mchumba wake.
Ahmed Abdirahman,27 anatuhumiwa kuiba pete hiyo ya dhahabu yenye thamani  ya Sh35, 000 za Kenya kutoka kwa  Kadar Mohammed siku ya  May 23 huko  Korogocho  Nairobi  nchini Kenya na baadaye kumvesha mchumba wake kwa madai kwamba amenunua kwa ajili yeke.
Kadar aliiambia mahakama kwamba walikuwa pamoja na Ahamad ambaye ni rafiki yake mkubwa katika mradi unaojishughulisha na vijana ndipo ahamad alipofanya tukio hilo.
Na alipojaribu kuumuuliza rafiki yake kama aliiona pete hiyo lakini Ahamad alikataa katakata kuiona pete hiyo.
Ilimbidi  awashirikishe na wazazi wake juu ya tukio hilo lakini aliendelea kukataa kwamba ajaiba pete hiyo.
Baadaye aliiona pete hiyo ikiwa imezaliwa na mchumba wa rafiki yake, yaani mpenzi wa Ahamad ndipo alipokwenda kuripoti police na kumsweka korokoroni.
Hata hivyo Ahamad alikataa mahakani mbele ya hakimu  Emilly ominde na kuachiwa kwa dhamana ya Sh. 10,000 mpaka kesi iatakaposikilizwa tena mwezi ujao.
Daily post

No comments: