HATIMAYE TIMU YA CHANG’OMBE FC YA NDUMBWE YATAWAZWA MABINGWA WAPYA WA
LIGI DARAJA LA NNE MTWARA VIJIJINI
![]() | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
New stars |
Mashabiki wa chang'ombe wakifurahiya ushindi wa timu yao
![]() | |||
Katibu wa chama soka Mtwara vijijini Selemai Samkwa kushoto akiwa na Ally Kumbo kulia wakifuatilia mechi |
![]() |
Mbuke Rashidi mchambuzi wa soka Pride Fm Radio naye alikuwepo |
Timu ya Chang’ombe FC ya Ndumbwe Mtwara vijijini leo hii imeibuka bingwa wa
ligi daraja la nne mtwara vijijini baada ya kuisambaratisha New stars ya Mbawala
kwa mabao 3-2 katika mchezo wa fainali uliofanyika katika uwanja wa Nagwanda
Sijaona Mjini Mtwara.
Mchezo wa huo ulivuta hisia za mashabiki wengi wa mtwara mjini na
vijijini kutokana na sakata la mchezaji Nalinga Ally Faki wa timu ya New Stars ambaye
alizua sintofahamu ndani ya uongozi wa chama cha soka mtwara vijijini MRDFA baada
ya mchezaji huyo kufungiwa mwaka mmoja kutocheza mpira wa miguu baada ya
kubainika kwamba alisajili timu mbili.
Lakini baadaye alifunguliwa na kamati ya nidhamu ambayo haikufahamika kamati
hiyo inaongozwa na nani, kabla ya adhabu yake kumalizika. Jambo ambalo lilizua
mgogoro baina ya viongozi wa chama hicho na hatimaye mwenyekiti wa chama hicho
Rashidi Chande kuingilia kati na kutengua matokeo ya mchezo nusu fainali ya
kwanza kati ya Shivo na New Stars ambao new stars ilishinda bao 1-0 na kuwapa
shivo pointi tatu na magoli 3 baada ya new stars kubainika kumchezesha mchezaji
Nalinga Faki kinyume na taratibu. Na katika fainali ya pili new stars
walifungwa mabao 3-1 hivyo kuwapa tiketi shivo kucheza fainali kutokana na
uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Hatimaye mgogoro huo uliendelea kufukuta na kusuluhishwa na kamati ya
nidhamu na haki za wachezaji ya chama cha soka Mkoani Mtwara MTWAREFA baada ya new stars kukata rufaa na
kushinda kucheza fainali na Chang’ombe.
Kwa mtokeo hayo timu za Chang’ombe Ndumbwe, New Stars na Chimbuko za mbawala juu zimepata
tiketi za kucheza ligi ya mkoa.
No comments:
Post a Comment