Sunday, April 27, 2014

AFCON 2015-MOROCCO: DROO YAFANYIKA
DROO ya Mashindano ya Mataifa ya Africa, rasmi kama Orange Africa Cup of Nations Morocco 2015, ambayo Fainali zake zitachezwa huko Morocco kati ya Tarehe 17 Januari hadi 8 Februari 2015, imefanyika hii Leo huko Cairo, Egypt.

Nchi 51 zitashiriki Mashindano haya ambapo Mauritania na South Sudan zilishinda toka Raundi ya Kwanza na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano ambayo Tanzania itacheza na Zimbabwe.

Washindi 14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano wataingia Raundi ya Tatu ya Mtoano ili kupata Timu 7 zitakazosonga kwenye Makundi ambayo hii Leo pia yamepangwa.

Ikiwa Tanzania itaitoa Zimbabwe basi kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano itacheza na Mshindi kati ya Mozambique na South Sudan na Tanzania ikipita hapo itaingia KUNDI F ambako ziko Zambia, Cape Verde na Niger.

Yapo Makundi 7 ambapo Mshindi wa Kila Kundi na Mshindi wa Pili wa Kila Kundi pamoja na Timu moja iliyofuzu Nafasi ya 3 Bora katika Makundi ndizo zitaingia Fainali kuungana na Morocco na kufanya idadi ya Timu 16 kwenye Fainali.

RATIBA/MAKUNDI:

Nchi ambazo zimeingia Makundi moja kwa moja: Nigeria, Ghana, Ivory Coast, Zambia, Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria, Angola, Cape Verde, Togo, Egypt, South Africa, Cameroon, DR Congo, Ethiopia, Gabon, Niger, Guinea, Senegal and Sudan.

RAUNDI YA PILI YA MTOANO

Mechi Na 1: Liberia vs Lesotho

Mechi Na 2: Kenya vs Comoros

Mechi Na 3: Madagascar vs Uganda

Mechi Na 4: Mauritania vs Equatorial Guinea

Mechi Na 5: Namibia vs Congo

Mechi Na 6: Libya vs Rwanda

Mechi Na 7: Burundi vs Botswana

Mechi Na 8: Central African Republic vs Guinea Bissau

Mechi Na 9: Swaziland vs Sierra Leone

Mechi Na 10: Gambia vs Seychelles 

Mechi Na 11: Sao Tome e Principe vs Benin

Mechi Na 12: Malawi vs Chad

Mechi Na 13: Tanzania vs Zimbabwe

Mechi Na 14: Mozambique vs South Sudan



Mechi za Kwanza 16,17,18 Mei 2014

Mechi za Marudiano 30,31 Mei au 1 Jun1 2014

No comments: