AFCON
2015-MOROCCO: DROO YAFANYIKA
DROO
ya Mashindano ya Mataifa ya Africa, rasmi kama Orange Africa Cup of Nations
Morocco 2015, ambayo Fainali zake zitachezwa huko Morocco kati ya Tarehe 17
Januari hadi 8 Februari 2015, imefanyika hii Leo huko Cairo, Egypt.
Nchi
51 zitashiriki Mashindano haya ambapo Mauritania na South Sudan zilishinda toka
Raundi ya Kwanza na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano ambayo Tanzania itacheza
na Zimbabwe.
Washindi
14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano wataingia Raundi ya Tatu ya Mtoano ili kupata
Timu 7 zitakazosonga kwenye Makundi ambayo hii Leo pia yamepangwa.
Ikiwa
Tanzania itaitoa Zimbabwe basi kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano itacheza na
Mshindi kati ya Mozambique na South Sudan na Tanzania ikipita hapo itaingia
KUNDI F ambako ziko Zambia, Cape Verde na Niger.
Yapo
Makundi 7 ambapo Mshindi wa Kila Kundi na Mshindi wa Pili wa Kila Kundi pamoja
na Timu moja iliyofuzu Nafasi ya 3 Bora katika Makundi ndizo zitaingia Fainali
kuungana na Morocco na kufanya idadi ya Timu 16 kwenye Fainali.
RATIBA/MAKUNDI:
Nchi ambazo zimeingia Makundi moja kwa
moja:
Nigeria, Ghana, Ivory Coast, Zambia, Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria,
Angola, Cape Verde, Togo, Egypt, South Africa, Cameroon, DR Congo, Ethiopia,
Gabon, Niger, Guinea, Senegal and Sudan.
RAUNDI
YA PILI YA MTOANO
Mechi Na 1: Liberia vs Lesotho
Mechi Na 2: Kenya vs Comoros
Mechi Na 3: Madagascar vs Uganda
Mechi Na 4: Mauritania vs Equatorial Guinea
Mechi Na 5: Namibia vs Congo
Mechi Na 6: Libya vs Rwanda
Mechi Na 7: Burundi vs Botswana
Mechi Na 8: Central African Republic vs Guinea
Bissau
Mechi Na 9: Swaziland vs Sierra Leone
Mechi Na 10: Gambia vs Seychelles
Mechi Na 11: Sao Tome e Principe vs Benin
Mechi Na 12: Malawi vs Chad
Mechi Na 13: Tanzania vs Zimbabwe
Mechi Na 14: Mozambique vs South Sudan
Mechi za Kwanza 16,17,18
Mei 2014
Mechi za Marudiano 30,31
Mei au 1 Jun1 2014
No comments:
Post a Comment