BABA ACHARUKA, ASITISHA HARUSI YA
BINTIYE ASIOLEWE NA MCHUNGAJI HUKO KENYA
![]() |
Jeff Wanjau na Alice Mukami |
KULIZUKA
kioja katika kanisa moja mjini Othaya, Jimbo la Nyeri, mzee aliposimamisha
harusi ya binti yake aliyepanga kuolewa na mpenzi wake ambaye ni kasisi.
Mzee
Peter King’ori alisimama harusi ilipokuwa ikiendelea katika kanisa la Prophetic
House of Mercy na kusema hangekubali binti yake aolewe na pasta huyo
Bw
Kingori alihutubia waliohudhuria harusi hiyo akisema hangeruhusu binti yake,
Alice Mukami, aolewe na Kasisi Jeff Wanjau kwa kuwa alikuwa ameoa mke mwingine
kisha akamuacha.
Alisema
alifahamishwa kuhusu harusi hiyo mnamo Ijumaa mwendo wa Saa Nne asubuhi na
akakasirika kusikia binti yake alipanga kuolewa na pasta huyo.
“Huyu
bwana harusi mnayemuona hapa alikuwa ameoa mwanamke mwingine na
akamuacha na siwezi kukukabali binti yangu aolewe na mtu ambaye kazi yake
ni kuoa wanawake kisha kuwaacha,” akasema Bw Kingori.
Aliongeza
kwamba kama angefahamu kuhusu mipango ya harusi mapema angeenda mahakamani
kupata agizo la kusimamisha wawili hao kuoana.
Ghafla
tu baada ya hotuba yake hiyo, Kasisi Wanjau na Bi Mukami walitoroka wakitumia
gari walilokodisha.
Akiongea
na wanahabari baadaye, Wanjau alikanusha madai ya mkwe wake akisema alikuwa
amemfahamisha kwamba alitaka kumuoa binti yake lakini akakataa.
Hata
hivyo alikiri kuwa alikuwa ameoa mke mwingine na wakazaa watoto wawili lakini
wakatalikiana baada ya kutofautiana.
Kasisi
huyo alisema ingawa harusi ilitibuka ataendelea kuishi na Bi Mukami kama mtu na
mkewe.
“Sioni
sababu yoyote ya kukosa kumuoa Bi Mukami kwa sababu nina cheti cha talaka kwa
mke wangu wa kwanza na sasa niko huru kuoa mwanamke yeyote ninayemtaka,”
akasema.
Aliongeza
kuwa harusi yao ilikuwa imekubaliwa na askofu wa kanisa lake ambaye alitangaza
kwamba Wanjau alitalikiana na mkewe na akampa idhini ya kuoa mke mwingine. Kwa
upande wake, Bi Mukami alisema haoni shida yoyote ya kuolewa na Kasisi Wanjau
kwa kuwa anampenda sana na hawezi kumuacha.
“Ninampenda
sana na sitamuacha hata kama wazazi wangu wanapinga harusi yetu. Tutaendelea
kuishi pamoja kwa sababu tumekubaliwa na kanisa letu,” akasema Bi Mukami.
Hata
hivyo, Kasisi Wanjau alisema yuko tayari kupatana na wakwe wakati wowote ule
hata kama atakuwa amemuoa binti yao.
Kusimamishwa
kwa harusi hiyo kulisababisha hasara kubwa huku chakula kilichotayarishwa
kikiharibika.
Umati
mkubwa wa watu waliofika kanisa kushuhudia walitawanyika na kwenda zao baada ya
harusi kutibuka.
No comments:
Post a Comment