UEFA CHAMPIONZ LIGI, VAN PERSIE AIPELEKA MAN UTD ROBO
FAINALI
Mabao
matatu yaani HETITRIKI ya Robin van Persie Usiku wa kuamkia leo huu imewapa
Manchester United ushindi wa Bao 3-0 dhidi ya Olympiakos na kutinga Robo
Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa Jumla ya Bao 3-2 katika Mechi mbili.
Hadi
Mapumziko, Man United walikuwa mbele kwa Bao 2-0, la kwanza likiwa kwa Penati
baada ya Van Persie kufanyiwa Faulo.
Huu
ni ushindi mkubwa kwa Mabingwa hao wa England hasa ukizingatia walikuwa
wamefungwa 2-0 katika Mechi ya Kwanza na pia Jumapili walichapwa na Liverpool
Bao 3-0 na kila Mtu alikuwa akimsakama Meneja David Moyes kwamba hana jipya.
DORTMUND 1 ZENIT 2
Wakicheza
kwao Signal Iguna Park huko Jijini Dortmund, Germany, Borussia Dortmund Usiku
wa kuamkia leo wamechapwa Bao 2-1 na Klabu ya Urusi, Zenit St. Petersburg ya
Urusi lakini wamefuzu kuingia Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa Jumla ya
Bao 5-4.Dortmund waliifunga Zenit Bao 4-2 huko Urusi katika Mechi ya Kwanza.
Bao za Zenit zilifungwa na Givaldinho Hulk, Dakika ya 16, na Jose Salomon Rondon, Dakika ya 73 wakati Bao la Dortmund Mfungaji alikuwa Sebastian Kehl katika Dakika ya 39.
TIMU ZILIZOTINGA ROBO FAINALI:
-Bayern
Munich
-Atletico
Madrid
-Barcelona
-Paris
Saint-Germain
-Chelsea
-Real
Madrid
-Manchester
United
-Borussia
Dortmund
No comments:
Post a Comment