Friday, February 28, 2014

DUNIANI KUNAVITUKO,MWANAMUME  AMTOA MKEWE KAMA MALIPO YA DENI
Moi’s Bridge,
MWANAMUME katika kijiji cha Lwanda, kata ndogo ya Moi’s Bridge, katika jimbo ndogo la Likuyani nchini Kenya ameshangaza wakazi baada ya kukataa kulipa deni la Sh900 na badala yake akamtoa mkewe kama malipo.

Kwa mujibu wa Patrick Andabwa, aliyekuwa akidai deni lake, alimsaidia mwanamume huyo kutengeneza matofali. Hata hivyo baada yake kumaliza kazi,alikataa kumlipa pesa zake na badala yake akamwambia amchukue mkewe.

Ingawa mimi bado ni kapera, nimeamua kumchukua na siangalii nyuma,” akasema mwanamume huyo wa umri wa miaka 22.

Mwanamke mhusika aliyetambuliwa kwa jina Jones Kevogo hakupinga mpango huo.

Alisema alikubali kwa sababu mumewe alikuwa na mazoea ya kuajiri wafanyakazi na kisha kukataa kuwalipa akidai kwamba walikuwa wameanzisha uhusiano wa kimapenzi naye.

 “Hii si mara ya kwanza,” akasema na kuongeza kuwa mwanamume huyo ametumia ‘mbinu’ hiyo mara kadha kukwepa kulipa madeni ya watu.

Jones,43, ambaye ni mama wa watoto watano alisema ameamua kuachana na aibu ya kuhusishwa na mumewe ambaye wameishi pamoja kwa miaka 20.

 “Nina matumaini kwamba ndoa yangu mpya itafanya kazi licha ya tofauti kubwa ya kiumri kati yetu,” akasema akidai kwamba alikuwa akidhulumiwa katika ndoa yake ya awali.

Alisema hatabadilisha uamuzi wake wa kumuacha mumewe hataka kama ndoa yake ya sasa itasambaratika. Alieleza kuwa watoto waliowazaa na mumewe wako huru kumtembelea.

No comments: