Sunday, January 19, 2014

UTAMADUNI NA MICHEZO.

Mbunge wa Kondoa Kusini (CCM) Juma Mkamia ametangazwa kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Nkamia anachukua nafasi ya Amos Makala ambaye amehamia katika wizara nyingine ya maji.

Nkamia aliyewahi kuwa Katibu Mwenezi wa Simba, ametangazwa leo wakati wa baraza jipya la mawaziri ambalo limetangazwa baada ya baadhi ya mawaziri kufutwa kazi na wengine kujiuzuru.

Nkamia ambaye taaluma yake ni mwandishi wa habari amewahi kufanya kazi ya utangazaji katika mashirika mbalimbali likiwemo Redio Tanzania, TBC na yale ya kimataifa kama BBC na Voice of America (VOA).

No comments: