UEFA CHAMPIONS LEAGUE PELLEGRINI ASALIMU AMRI, ROBBEN ASEMA CITY NI WEPESI
BAADA
ya Jana kumalizika kwa Mechi za Pili za Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL,
huku maneno makubwa yakiwa kipondo cha Bao 3-1 walichoshushiwa Manchester City
Nyumbani kwao Etihad na Mabingwa wa Ulaya Bayern Munich na pia Wadau kuiona Man
United ikitoka Sare ya Bao 1-1 Ugenini huko Donetsk, Nchini Ukraine, dimba
ambalo Chelsea na Arsenal walikiona cha Mtema Kuni, yafuatayo ni maoni ya
baadhi ya Wadau.
PELLEGRINI NA KICHAPO
Mabingwa
Bayern Munich walitoa somo kubwa la Kandanda safi kwa kuichapa Man City Uwanja
kwao Etihad Bao 3-1 katika Mechi ya Kundi D la UCL huku Bao hizo zikipigwa na
Franck Ribery, Thomas Muller na Arjen Robben na City wakifunga Bao lao kupitia
Alvaro Negredo.
Mechi
hii ilishuhudia makosa makubwa ya Kipa wa Man City, Joe Hart, ambae ndie Kipa
Nambari Wani wa England, na pia Kadi Nyekundu kwa Jerome Boateng wa Bayern.
Matokeo
haya yamewafanya Bayern Munich wawe kileleni mwa Kundi D na kuwaacha Man City
na CSKA Moscow kugombea Nafasi ya Pili.
Meneja
wa Man City, Manuel Pellegrini, amekiri: “Tulicheza vibaya sana. Bayern, kama
Siku zote, walicheza vizuri mno. Tumepata somo kubwa toka Magoli yao. Hatukuwa
na nafasi tukiwa na Mpira miguuni kwetu.”
Pellegrini
pia alikiri kukerwa na fomu ya Kipa wake Joe Hart na kusema: “Ni kweli nina
wasiwasi na makosa lakini hiyo haikuwa Gemu rahisi!”
PEP GUARDIOLA
Pep
Guardiola, Meneja wa Bayern Munich, alisema: “Nilisema Jana na sijabadilika.
Man City wataingia Raundi ijayo na ni wapinzani wagumu kwa Timu yeyote.
Tulicheza vizuri, tumeshinda na Soka ni spesho. Nina bahati kuwa na Wachezaji
hawa. Ni safi kuja kwenye Nchi hii, wanayopenda sana Soka, na kucheza vizuri
kama leo.”
ARJEN ROBBEN
Arjen
Robben, ambae alifunga Bao moja kwa Timu yake Bayern Munich, alisema:
"Tulitawala dhidi ya Timu kubwa Ulaya. Hatukutegemea Gemu nyepesi na rahisi
kama ile!”
GARY NEVILLE
Gary
Neville, ambae ni Kocha Msaidizi kwenye Timu ya Taifa ya England na pia
Mchambuzi wa Soka kwenye Kituo cha TV cha SKY, mara baada ya Joe Hart kuruhusu
Bao la Dakika ya 7 la Shuti la mbali la Franck RibĂ©ry, alisema: “Ni shuti la
nguvu. Joe Hart alitakiwa kucheza vizuri zaidi, amefungwa kwenye Posti ya
karibu yake, Mpira umempenya mikononi. Si mwanzo mzuri kwa Man City na Kipa.”
Baada
ya Bao la Dakika ya 60 la Arjen Robben, Neville alisema: “Unaweza kusema Joe
Hart alitakiwa kucheza vizuri tena. Amefungwa tena kwenye Posti ya karibu yake.
Hii ni mara ya pili sasa. Lazima atahuzunika.”
MAN UNITED NA SARE
DANNY WELBECK
Danny
Welbeck, ambae ndie aliefunga Bao walipotoka droo 1-1 na Shakhtar Donetsk huko
Ukraine hapo Jana Usiku, anaamini huu ni wakati wa Manchester United kuwa
pamoja baada ya mwanzo mgumu kwa Meneja wao mpya David Moyes.
Sare
hiyo imewafanya Man United wabaki kileleni mwa Kundi A la UCL wakiwa na Pointi
4 sawa na Shakhtar Donetsk lakini wao wako juu kwa ubora wa Magoli.
Moyes
amekuwa kwenye presha baada ya Jumamosi iliyopita kufungwa Old Trafford na West
Bromwich Albion Bao 1-0 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England lakini Jana walicheza
vizuri dhidi ya Timu ambayo haijapoteza kwao ikicheza na Timu za England na
Jana Shakhtar walinusurika baada kusawazisha Bao Dakika 14 kabla Mpira kwisha
kwa Bao la Taison.
Welbeck
alinena: "Yalikuwa si matokeo mabaya. Sidhani kama kuna Timu nyingi
zimekuja hapa na kupata Pointi 3. Pointi 4 kwa Mechi mbili si mbaya. Ni wazi
sisi ni Manchester United na tunataka kushinda kila Gemu. Lakini kupata Pointi
1 hapa inaridhisha. Mambo hayendi vyema kwenye Ligi lakini lazima tuwe pamoja
na kutilia mkazo Gemu yetu ijayo tu na si mbele.”
DAVID MOYES
Nae
Meneja David Moyes, mara baada ya Mechi na Shakhtar, alizungumza: “Ni Pointi
nzuri kwenye UCL kuipata hapa. Inabidi tushinde Gemu nyingine ili tusonge!”
Ukiondoa
Sare ya Jana, Shakhtar walishinda Mechi zao zote 3 zilizopita kwenye UCL dhidi
ya Klabu za England zilizochezwa Donetsk kwa kuzifunga Chelsea Msimu wa 2012/13
na Arsenal Misimu ya 2000/01 na 2010/11.
MIRCEA LUCESCU
Kocha
wa Shakhtar Donetsk, Mircea Lucescu, Mkongwe wa Miaka 68 ambae yuko na Klabu
hiyo tangu 2004, amekubali Sare ilikuwa Matokeo yanayoridhisha pale aliposema:
“Tuliwaruhusu Man United kupata Bao la mapema na ilibidi tuhangaike
kusawazisha. Sare hii ni Matokeo yanayoridhisha yanayofanya Klabu zote ziwe na
nafasi nzuri kusonga.”
Man
United sasa inakabiliwa na Mechi mbili mfululizo dhidi ya Real Sociedad ambao
wako mkiani mwa Kundi A baada kuchapwa Mechi zao zote mbili dhidi ya Shakhtar
na Bayer Leverkusen.
No comments:
Post a Comment