KENYA YARUHUSIWA KUANDAA MICHUANO YA CHALLENGE
![]() |
Mwenyekiti wa FKF Sam Nyamweya |
KAMATI
ya Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limetoa kibali kwa
Kenya kuandaa michuano ya Senior Challenge Cup mwaka huu.
Katibu
Mkuu wa CECAFA ameondoa wasi wasi wa awali kwamba michuano hiyo inaweza isifanyike
nchini Kenya kutokana na mvutano kati yake na mwenyekiti wa Shirikisho la Soka
Kenya (FKF), Sam Nyamweya.
“Kwa
hakika sivutani na Nyamweya. Ningependa kuwahakikishia Kenya kwamba mechi za
Senior Challenge zitafanyika Kenya na tayari tumeanza kutafuta mdhamini mkuu,”
alisema Musonye katika mkutano na waandishi wa habari.
Hata
hivyo, Musonye alisema aliamua kuinyima Kenya nafasi hiyo mwaka uliopita, kwa
lengo la kutaka zifanyike nchini mwaka huu taifa linaadhimisha miaka 50 tangu
Kenya ipate uhuru.
“Nilikuwa
na mawazo mazuri kwa sababu sasa yatakuwa mashindano ya hali ya juu kwa vile
yataenda sambamba na sherehe za kuadhimisha miaka 50 za uhuru wa Kenya,”
alisema.
“Itabidi
hata Serikali itambue mashindano hayo,” aliongeza.
Nyamweya
alisema kwa mara ya kwanza, uwanja wa Kenyatta Stadium mjini Machakos utaandaa
baadhi ya mechi za mashindano hayo ya kimataifa.
Alisema
ukarabati katika uwanja huo unaendelea ili uweze kukaliwa na mashabiki 8,000.
“Tunataka
kupeleka boli mashinani na tumetambua Machakos kama mojawapo wa viwanja
vitakavyotumika mwaka huu,” alisema Nyamweya.
Alisema
viwanja vingine ni Kisumu Moi Stadium ambao utakuwa umekamilika kabla ya mechi
hizo kuanza Novemba 27 na kuendelea hadi Desemba 12.
“Kadhalika
kuna Mumias Complex na Afraha Stadium,” aliongeza.
Alisema
tayari Magavana wa eneo hizo wamejumuishwa katika kamati andalizi wa michuano
hiyo itakayoshirikisha timu 12.
Waliokuwa
mabingwa wa Afrika, Zambia na Malawi zimealikwa kutoka nje ya jimbo la CECAFA.
Nyamweya
alisema lengo la mashindano ya mwaka huu ni kuleta amani barani Afrika.
“Tunataka
kutumia mashindano haya kuleta amani nchini Somalia. Tutafanya maandamano ya
amani kabla ya mechi hizo kuanza,” alisema Nyamweya.
Rais
wa CAF, Issa Hayatou anatarajiwa kuwa mgeni wa heshima wakati wa mashindano
hayo.
Nchi
12 zilizothibitisha kushiriki ni wenyeji, Kenya, mabingwa watetezi Uganda,
Tanzaania, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Sudan Kusini, Sudan, Somalia, Eritrea,
Djibouti na Zanzibar.
Kenya
ilikuwa muandalizi kwa mara ya mwisho mnamo 2009.
No comments:
Post a Comment