Thursday, September 26, 2013

MAN UTD YAMALIZA HASIRA KWA LIVERPOOL, YAICHAPA 1-0 KOMBE LA LIGI, SASA KUVAANA NORWICH,ASERNAL KUVAANA NA CHELSEA RAUNDI YA NNE, NEW CASTLE NA MAN CITY
 
Timu ya Manchester United imeibamiza timu ya Liverpool bao 1-0 katika mchezo wa kombe la ligi na kufuta machungu ya kufungwa na Manchester City mabao 4-1 mwishoni mwa wiki katika ligi kuu nchini  ungereza.

Katika mchezo huo macho yote yalikuwa kwa Luis Suarez baada ya kurejea Liverpool kufuatia kumaliza adhabu yake ya mechi 10, lakini Javier Hernandez ndiye aliyeiua liverpool kwa bao lake pekee lililoipeleka Manchester United Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One.
Hatimaye Suarez alicheza mechi yake ya kwanza ya msimu mpya baada ya kumaliza kutumikia adhabu yake ya kumng'ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic msimu uliopita.
Na wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay alizomewa na mashabiki Uwanja wa Old Trafford, alikuwa ni Chicharito aliyepoza maumivu ya David Moyes kufuatia kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa wapinzani, Manchester City katika Ligi Kuu Jumapili.
Nayo Klabu  ya Arsenal itamenyana na wapinzani wao katika Jiji la London, Chelsea katika Raundi ya Nne michuano hiyo baada ya kuitoa West Brom kwa penalti 4-3 Uwanja wa Hawthorns.
Mechi hiyo ilisha kwa sare ya 1-1 usiku wa leo. Manchester United baada ya kuwatoa wapinzan wao, Liverpool watamenyana na Norwich nyumbani katika Raundi ya Nne.
Birmingham iliyowatoa mabingwa watetezi Swansea kwa mabao 3-1 watacheza tena nyumbani katika 16 Bora, safari hii wakimenyana na timu ya Mark Hughes, Stoke.
Licha ya kupangiwa wapinzani wagumu, lakini The Blues bado wanapewa nafasi kubwa ya kutwaa tena taji walilolitwaa mwaka 2011, na United ikiwa timu nyingine inayopewa nafasi pia baada ya kupangiwa Norwich.
Katika mechi nyingine, Newcastle itaikaribisha Manchester City Uwanja wa St James Park baada ya kuwatoa Leeds, wakati Hull wataifuata Tottenham siku kadhaa baada ya kucheza mechi ya Ligi Kuu, Uwanja wa White Hart Lane.
Timu isiyo na kocha kwa sasa, Sunderland itamenyana na Southampton, wakati West Ham watakwedna Kaskazini kumenyana na Burnley.
Fulham ya Martin Jol itaifuata Leicester kusaka nafasi ya Robo Fainali.

No comments: